RAIS Jakaya Kikwete amestushwa na kuvurugwa kwa mpango wa ujenzi wa
nyumba za watendaji wa Kijiji cha Msoga mkoani Pwani, tofauti na
makubali...ano na wanakijiji wa kijiji hicho miezi michache iliyopita.
Akizungumza jana katika kambi ya mafunzo ya vijana zaidi ya 400
iliyoasisiwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza, Rais Kikwete
alisema ameshangazwa na mabadiliko hayo aliyoyaelezea kuwa ni kinyume
na makubaliano ya wanakijiji wa Msoga.
“Nilipokuwa nakuja huku
kwenye hii kambi, nilijua kwamba ujenzi wa nyumba za watendaji wa
tarafa hii, ungekuwa upande ule (akionyesha upande wa pili wa
barabara), lakini nashangaa misingi ya nyumba imeanza kuchimbwa huku,
ni kinyume kabisa cha makubaliano yetu,”alisema Kikwete.
Alisema kuwa anashangazwa na mabadiliko hayo yaliyofanywa kinyume na
mpango ambao yeye kama mwanakijiji wa kijiji hicho na wenzake
walikubaliana ambapo amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Pwani kulifanyia kazi
suala hilo.
“Mama Mahiza ni nini kimetokea hapa, mbona imeenda
kinyume kabisa na tulivyokubaliana, si mmeona hapa jamani?,” alisema
Kikwete akihoji na kuongeza:
“Sisi huwa hatujengi eneo hili,
ni udongo wa mfinyanzi mkali ambao wakati wa mvua ni tope na wakati wa
kiangazi ni jiwe, hebu angalieni bwana.”
Source: Mwananchi Newspaper
Never afraid to try on your own; No matter what, you can keep it real. Trust yourself...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?
Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...

-
Ee Mungu Mwenyezi uliyekubali Mwanao Yesu Kristu ateswe mpaka kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zangu naomba uwe nami. Ee Msal...
-
Baada ya miaka 13 ya kuwapo katika fani ya sanaa ya maigizo, hakuna shaka kwamba, Ste...
No comments:
Post a Comment