25 March, 2014

MACHOZI YATAWALA VIFO VYA ABIRIA MALAYSIA

Kufuatia tukio la taarifa za awali kuhusu kupotea kwa ndege ya shirika la Malaysia airlinesaina ya Boeing yenye namba 777 MH370 nchini Malaysia kwa takribani siku 16 hadi sasa, hatimaye Waziri mkuu wa Malaysia Bw. Najib Razak ametoa taarifa ya awali kuhusiana na ndege hiyo.

Ripoti hiyo iliyosomwa na waziri huyo, inasema kuwa ndege hiyo ya Malaysia airlines ilidondoka kusini mwa bahari ya Hindi huku ikielezwa kuwa hadi sasa hakuna matumaini ya kupona kwa abiria waliokuwamo katika ndege hiyo.

Ikumbukwe kuwa, ndege hiyo ilitaarifiwa kupotea tangu marchi 8 2014 ikitokea Kuala Lumpur huku ikiwa na jumla ya abiria 239.Na hadi sasa shughuli ya kuipata miili ya marehemu hao inaendelea kufanyika. Hivyo basi endelea kukaa karibu na www.msombe.blogspot.com kwa taarifa zaidi.
Hapa chini ni baadhi ya picha za wanandugu wakiomboleza kwa uchungu kufuatia tukio hilo.





No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...