24 April, 2014

BREAKING NEWS : BOMU LALIPUKA KENYA NA KUUWA POLISI NA ABIRIA WALIOKUWA NA BOMU HILO


Bomu linaripotiwa kulipuka kwenye gari na kuuwa watu wanne ikiwa ni Polisi wawili na abiria wawili ambao wanashukiwa walikuwa na bomu hilo kwenye gari karibu na kituo cha Polisi cha Pangani.
Lakini ilivyotokea inaripotiwa na gazeti la Starndard kwamba Polisi hao wawili waliwakamata washukiwa waliokuwa na kuamua kuwapeleka kituo cha Polisi wakiwa na bomu hilo kwenye gari!
Kabla ya kufika kituoni bomu hilo lilipuka na kuuwa wote Polisi pamoja na washukiwa ambao walikuwa kwenye jaribio la kujitoa muhanga.Haijajulikana mara moja kwanini Polisi hao waliamua kuchukua hatua ya namna hii lakini habari zaidi baadaye..


No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...