“Najua
 kuna maneno mengi kuhusu suala hili. Kwa hiyo maelekezo yangu ni kwamba
 kaeni chini, mjadili matatizo yaliyopo na kupata ufumbuzi. Kama ni 
suala la bei pia linazungumzika lakini tunahitaji mfumo huu wa malipo ya
 kodi,” alisema.
Aliagiza
 viongozi wa TRA kukaa chini na wadau na watumiaji wa mashine hizo 
kuzungumza na kutafuta majawabu yanayolalamikiwa na wadau.
Alisema
 kuacha kutumia mashine hizo ni kurudi nyuma kwa kuwa zimeshaanza 
kutumika duniani kote na hata nchi jirani baadhi zimeshaanza kutumia na 
nyingine ziko katika maandalizi ya kutumia.
“Kwenye
 hili tusirudi nyuma kwa sababu tukifanya hivyo, tutakuwa tunarudi nyuma
 sana kwa sababu dunia nzima inaelekea huko na hata majirani zetu wote 
ama wameanzisha mfumo huo ama wanajiandaa kuuanzisha.”
“Hatuwezi
 kurejea kwenye mfumo ule wa kutumia vijirisiti. Mfumo wa sasa unaifanya
 kazi ya kukusanya kodi kuwa rahisi kwa Serikali yenyewe na kwa walipa 
kodi. Najua watu hawapendi kulipa kodi lakini hakuna njia ya jinsi ya 
kuendelea isipokuwa kwa kulipa kodi,” alisisitiza Rais Kikwete.
Kwa
 muda mrefu TRA imekuwa ikisisitiza kuwa utaratibu wa kutumia mashine za
 EFDs ulianzishwa kwa lengo la kumrahisishia mfanyabiashara utunzaji wa 
kumbukumbu za biashara za kila siku pamoja na kuondoa usumbufu wakati wa
 ukadiriaji wa kodi. Mfumo huo wa kutumia mashine za kodi za 
kielektroniki ulianza kutekelezwa kwa awamu.
Awamu ya kwanza ilianza mwaka 2010 kwa wafanyabiashara waliosajiliwa kwenye kodi ya ongezeko la thamani (VAT).
Awamu
 ya pili ilianza 2013 ikiwahusu wafanyabiashara ambao hawajasajiliwa 
kwenye VAT ambao mauzo ghafi kwa mwaka ni Sh milioni 14 na zaidi.
Kwa
 mujibu wa taarifa za TRA, wafanyabiashara zisizo rasmi zikiwemo za mama
 lishe na wale wanaotembeza bidhaa barabarani, hawahusiki kwa sababu 
hawana sehemu maalumu ya kufanyia biashara.
Miongoni
 mwa wafanyabiashara wanaotakiwa kutumia mashine hizo ni wenye maduka ya
 vipuri, mawakili, maduka ya jumla, wafanyabiashara wakubwa wa mbao, 
migahawa mikubwa, maduka ya simu na vipuri vyake, baa na vinywaji 
baridi, studio za picha, biashara za kutoa huduma za chakula, wauzaji wa
 pikipiki, maduka makubwa ya nguo na biashara zinginezo Kwa mujibu wa 
taarifa za TRA, kwa nchi nzima walengwa ni wafanyabiashara laki mbili tu
 kwa awamu ya pili kati ya wafanyabiashara zaidi ya milioni moja na nusu
 ambao wamesajiliwa kulipa kodi.
Rais
 Kikwete alikuwa katika ziara ya siku moja kukagua shughuli za maendeleo
 wilayani Karatu katika Mkoa wa Arusha na leo atafanya ziara kama hiyo 
ya siku moja katika Wilaya ya Mwanga, Mkoa wa Kilimanjaro.  
No comments:
Post a Comment