24 September, 2014

ANGALIA NYUKI WALIVYOWATIMUA WACHEZAJI MTIBWA, CAMERAMAN WA AZAM TV

Nyuki bana, nao wana yao. Katika mechi ya Ligi Kuu Bara, Jumapili iliyopita wakati Mtibwa Sugar ikiivaa Yanga, waliwakimbiza wachezaji wa Mtibwa. Wachezaji hao walikuwa wanashangilia bao lililofungwa na mwenzao Mussa Hassan Mgosi, ghafla nyuki hao wakaibuka na wachezaji hao wakalazimika kutimua mbio.
Cameraman wa Azam FC na mwenzake, pia walilazimika kuacha kazi yao na kutimua mbio baada ya lundo hilo la nyuki kuungana nao wakati wakishangilia. Hata hivyo halikuwa tukio la muda mrefu, nyuki hao ‘walichukua za time’. Mechi hiyo ya Ligi Kuu Bara iliisha kwa Mtibwa Sugar kushinda kwa mabao 2-0 kwenye uwanja wa Jamhuri.
Picha na salehjembe

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...