04 December, 2014

NDEGE YA KDF YAANGUKA KISMAYU SOMALIA

Ndege aina ya helicopter ya jeshi la Kenya
Ndege ya jeshi la KDF nchini Kenya imeanguka katika eneo la Kismayu nchini Somali.
Ndege hiyo ilianguka siku ya alhamisi mwendo wa saa tisa na robo ilipokuwa ikirudi Kenya baada ya kutekeleza mashambulizi katika eneo la Jamaame kusini mwa Somali.
Kulingana na msemaji wa Jeshi kanali david Obonyo: Ndege ya KDF iliokuwa ikirudi nchini Kenya baada ya kufanya mashambulizi katika eneo la Jamaame kusini mwa Somali,ilikumbwa na matatizo ya kiufundi na kuanguka katika eneo la Kismayu .
Kanali Obonyo hatahivyo hakusema iwapo kulikuwa na majeruhi yoyote.

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...