12 February, 2011

Uozo! Uozo mtupu!

Kauli yangu ya kila siku ya madaraka sasa yaachiwe wanawake ina kila mantiki ya kunifanya niandike waraka huu! Jamani Tanzania yetu leo si ya kufukia vichanga katika shimo moja bila chembe ya huruma!! Wanaume!! Kati ya watu waliohusishwa kwa asilimia zote na uhalifu huu ni wanaume!! Akiwemo kiongozi wa chumba cha kulaza maiti na mmiliki wa shamba lililofukia vichanga hao.
MAJI, UMEME: Ni kilio cha  watanzania walio wengi. Eti tuilipe Dowans! Jamani ninyi wanaume mliopewa madaraka kwa kuaminiwa vipi? Imekuaje? Hivi mnafahamu ni kwa kiasi gani taifa linaingia hasara kwasababu yakukosekana kwa huduma ya maji na umeme? Mlishawafikiria wale wanaojipatia riziki yao ya siku kwa kufanya shuhuli za saluni, kapenta, kuchomea na nyingine nyingi zinazotegemea umeme? Au mnataka watu wakabe, waue ili wajipatie riziki? Maji nayo yamekua gumzo!! Eti bomba linafanyiwa marekebisho! Khaa... mnashindwa kujifunza japo kwa wa Zanzibar ambao kwao maji ni bure!
TAHADHARI, CHUKUA HATUA

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...