Kama ni mfuatiliaji mzuri wa makala mbalimbali zinazihusu maswala ya
afya, magonjwa mbalimbali ya kuambukiza ikiwa ni pamoja na ugonjwa
unaoonekana kutopatiwa dawa kwa miaka zaidi ya 30 sasa tangu umeanza
kuathiri watu (UKIMWI) ukiendelea kuua mamia kwa maelfu duniani
utagundua kwamba kuna uwezekano mkubwa sana dawa hiyo ipo na watu
walishaigundua lakini kuna uwezekano kwamba kuna watu fulani wanaizuia
kwa sababu wananufaika kupitia watu kuendelea kuambukizwa gonjwa hili
hatari linaloangamiza wengi hasa katika nchi za Afrika zilizoko kusini
mwa Jangwa la Sahara.
Hata hivyo kuna uwezekano mkubwa sana kwamba ukimwi ulitengenezwa na
watu kwa makusudi Fulani, lakini kuna madaktari wengi kutoka pande zote
za dunia ambao karibu kila mwaka huwa wanakuja na matokeo Fulani baada
ya kufanya tafiti kwa muda mrefu zinazoleta matumaini makubwa kwamba
sasa dawa inaenda kupatikana lakini ghafla hawasikiki tena na badala
yake wanaibuka wengine namna hiyo, kama ilivyotokea miaka ya hivi
karibuni Israel, Marekani na hata Korea ya Kusini kuweza kugundua dawa
zilizofanyiwa majaribio na nyingine zilizo tayari zikisubiri tu
kujaribiwa kwenye mwili wa binadamu lakini ghafla hakuna kinachosikika
tena!
Wataalamu wanasema kuweza kupata dawa hii kunahitaji pesa nyingi sana za
kufanyia utafiti ikiwa ni pamoja na wataalamu wengi kushirikiana ila
pesa ambayo huwa inatolewa ni kidogo na hakuna ule ushirikiano wa
kutosha, ni kwa nini? Tumeshuhudua ndugu zetu wengi wakipoteza maisha,
watoto yatima wakiongezeka mitaani nguvu kazi ya taifa kupotea ikiwa ni
pamoja na viongozi wakubwa serikalini kwa sababu hii sasa ni kwa nini
nguvu nyingi zisiongezwe katika kutafuta tiba au angalau chanjo ili
kupunguza hii hali ambayo inazidi kuwa ya hatari?
Gazeti la Mwananchi la tarehe 10 Desemba ya mwaka 2011 lilitoa taarifa
ya utafiti uliofanywa baina ya hospitali ya KCMC ya mjini Moshi mkoani
Kilimanjaro kwa ushirikiano na chuo kikuu cha afya cha Duke cha nchini
Marekani juu ya uwezekano wa kupatikana chanjo na tiba ya ukimwi.
Utafiti huo uliofanywa na Dk Reddy akishirikiana na wataalamu wa hapa
nchini, Profesa Noel Sam, Profesa Saidi Kapiga na Sarah Chiduo,
ulibaini kuwa kuna watu ambao baada ya kuambukizwa VVU miili yao imeweza
kutengeneza kinga imara ambazo zimeweza kudhibiti kabisa virusi na wala
hawahitaji kutumia dawa za kupunguza makali ya ugonjwa huo maarufu kama
ARV.
Dk Reddy alisema watakachofanya kwenye utafiti wao, ambao
uliwahusisha pia wanasayansi wa nje ya nchi; Profesa John Bartlelt na
Profesa John Crump, ni kutengeneza chanjo ambayo itawafanya watu wote
kuwa na uwezo wa kutengeneza kinga hizo. Chanjo hiyo alisema kwa upande
mwingine wanategemea itakuwa ni tiba.
Alisema tafiti nyingi ambazo tayari ziko kwenye mchakato zinaweza kuzaa matunda ndani ya kipindi cha miaka saba ijayo.
Cha msingi nafikiri tujaribu kuondoa ile imani ya kwamba dawa ya ukimwi
haipo wala haiwezi kupatikana na kujaribu kushinikiza utafiti zaidi na
kufuatilia matokeo ya tafiti hizo na kuielimisha zaidi jamii juu ya
maswala yote ya afya, athari zake na hatua zilizofikiwa hizo ni sambamba
na harakati za kupunguza umaskini na majanga mengine yanayokumba jamii
mbalimbali hasa katika hizi nchi maskini na zinazoendelea.
Source: View TZ
Never afraid to try on your own; No matter what, you can keep it real. Trust yourself...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?
Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...

-
Ee Mungu Mwenyezi uliyekubali Mwanao Yesu Kristu ateswe mpaka kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zangu naomba uwe nami. Ee Msal...
-
Baada ya miaka 13 ya kuwapo katika fani ya sanaa ya maigizo, hakuna shaka kwamba, Ste...
No comments:
Post a Comment