Wasanii
mashuhuri wa sanaa ya filamu hapa nchini Jacob Steven 'JB' na mwanadada
anayeng'aa Aunt Ezekiel wamepata ulaji na kampuni ya ZUKU ambayo
inahusika na maswala ya ving'amuzi vya Tv zikiwemo channel ambazo
zinaonesha filamu za Kitanzania kwa sasa. Wasanii hao wamechaguliwa na
kampuni hiyo kuwa mabalozi wao kwa upande wa tasnia ya filamu na nchi ya
Tanzania kwa ujumla ambao sasa filamu zao zitakuwa zikioneshwa kwenye
king'amuzi cha kampuni hiyo huku nyingi zikiwa kutoka kwa wasambazaji
mahiri hapa Tanzania wanaojulikana kama
Steps Entertainment ya jijini Dar es salaam ambapo
lengo jingine la kufanya hivyo ni kuikuza lugha ya Kiswahili kupitia
filamu zetu hapa nchini ambazo zitakuwa zikionekana dunia nzima kwa
sasa. Never afraid to try on your own; No matter what, you can keep it real. Trust yourself...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?
Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...

-
Ee Mungu Mwenyezi uliyekubali Mwanao Yesu Kristu ateswe mpaka kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zangu naomba uwe nami. Ee Msal...
-
Baada ya miaka 13 ya kuwapo katika fani ya sanaa ya maigizo, hakuna shaka kwamba, Ste...
No comments:
Post a Comment