04 August, 2012

MSANII ROMA APATA AJALI YA GARI,AGONGANA NA FUSO!!



 













Majira ya mchana leo msanii wa muziki wa kizazi kipya Roma Mkatoliki amepata ajali ya gari baada ya gari alilokuwa akisafiria kutoka jijini Dar es salaam kwenda Morogoro kupata pancha na kuhama njia yake hali iliyosababisha gari hilo kugongana na gari jingine aina ya Fuso. Msanii huyo alikuwa akiendesha gari lake kwenye mwendo wa kawaida lakini ghafla tairi ya gari lake ilipata pancha na kupelekea ajali hiyo, Msanii huyo alikuwa anaenda kwenye show yake mjini huko akiwa na rafiki zake na hakuna yeyote aliyeumia wala kufariki kwenye ajali hiyo.


 
Hapa akitoa maelezo kwa polisi,

Gari hiyo baada ya ajali,

Baadhi ya rafiki wa Roma waliokuwa kwenye gari hiyo,



CHANZO; Djchoka

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...