Wana Ccm sasa wamehakikisha, wametambua, wameelewa kuwa siasa za kanda
ya kaskazini ni siasa nyingine si linganifu na siasa za pahala pengine.
Ushindi wa viti vinne vya udiwani kwa Chadema si USHINDI mkubwa kwao
kwani walijua UCHAGUZI ule ulikuwa mechi ya nyumbani, na kurudia
UCHAGUZI ule ulitokana na maamuzi yao ya kuwafukuza madiwani
wa chadema kwa kukaidi maagizo HALALI ya kamati kuu ya chadema. Na
walifikia maamuzi hayo magumu wakijua kabisa hata uchaguzi ungerudiwa
siku yeyote wangeshinda tu! Swali la kujiuliza ni kwanini chadema
wanajeuri ya kisiasa Arusha? Majibu yanaweza kuwa mengi kila mtu na lake
lakini jibu la msingi ni kuwa wana Arusha wanauelewa mpana,
wameelimishwa na wakaelimika, wmefundishika kuwa serikali tulivu ya CCM
iliyokaa madarakani kwa miaka 50 ndiyo chanzo kikubwa cha UMASKINI wao.
Wao kukosa Huduma ya afya bora, elimu bora, miundombinu ya barabara
bora, kupanda kwa gharama za maisha zinatokana serikali ya Ccm. Na
wakaelezwa kuwa fedha zao zinazoibwa kupitia miradi mbalimbali Kama EPA,
DEEP GREEN, KAGODA, DOWANS, MEREMETA n.k zinatumiwa na viongozi wa
serikali ya Ccm na familia zao huku wakiacha maelfu ya Watanzania wakifa
kwa kwashakoo, utapyamlo, wakifa kwenye foleni ya matibabu kwa kukosa
elfu mbili ya kununua dawa ya kuharisha! Huku viongozi wao wakipigana
vikumbo uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere wakielekea hospitali yao ya
rufaa Apollo nchini India kutibiwa malaria huku wakiambatana na
mashosti, ndugu jamaa na marafiki. Wana Arusha wanajua kuwa mashangingi
ya viongozi wao yanauzwa milioni 80 lakini viongozi wa Ccm wameengeza
mpaka yamefikia milioni Mia tatu, Pesa ya mlipa kodi! Wameelezwa na
viongozi wengine( HOSSEA) kuwa serikali haitaki kuwafikisha mahakamani
viongozi wala Rushwa, Mafisadi. Wanajua Tz ndio nchi pekee ambayo mwizi
anapewa mda wa kutafakari, kujitathimini ili arudishe fedha alizoiba!
Cha kushangaza Ccm wanamtuma MWIGULU NCHEMBA, SHONZA, MWAMPAMBA, kwenda
kuwaeleza wakazi wa Arusha kuwa chanzo cha matatizo yao, umaskini wao
ni kwa sababu ya MAANDAMANO, LEMA na CHADEMA!!. Wakasahau kuwa wapiga
kura wa Arusha wanaojitambua, wanajiielwa na kuwa adui wao namba moja ni
CCM na serikali yake! Mbaya zaidi vikafanyika vikao vya hadharani na
faragha vya kueneza uwongo kuwa Arusha haitaendelea kwani chadema wapo
nyuma ya mabomu, mauaji, ukatili, umwagaji wa Tindikali. Wakaendelea
kuwachonganisha na Wamasai mpaka ikafika hatua kikao cha ma-LAIGWANANI
kikaitishwa chini ya ufadhili wa Ccm wakatangaza kuwa watawafukuza
WACHAGGA Arusha kwa sababu wanaleta fujo, maandamano pasipo kujua mbinu
ile ilikuwa chafu kwani hata WACHAGGA ambao ni Ccm hawakupigia CCM kura
kwa hasira. Wana Arusha wanajua kuwa CHADEMA ni Chama kilichowakomboa
kifikra, ni chama pekee kinachoifanya serikali kuwajibika kwa wananchi,
ni chama kinachotetea maslahi mapana ya taifa, ni chama
kinachojitanabaisha na wananchi. Ccm hata waende taifa gani kumpata
mshauri mwenye shahada za uzamivu Mia Tisa, vyeti vya propaganda tani
nne. Kamwe hawataweza kuwashawishi wana Arusha kuwa CHADEMA ni chama
hatari, Chama cha matukio, chama cha maandamano, chama cha kidini, chama
cha WACHAGGA na kadhalika. Ccm wao waharakishe maendeleo kwa wana
Arusha wajenge miundombinu bora, watoe huduma ya afya bora, elimu bora
hakuna mtu atatafuta mbadala wa CCM. SHONZA, MWAMPAMBA, MWIGULU hawawezi
kubadilisha watu wanaojitambua kwa Kutoa matusi, kejeli na kutoa kauli
tata kuwa msipoichagua Ccm watakiona cha MOTO,
NICHUNGU LAKINI DAWA
(Kidumu Chama tawala CCM)
Never afraid to try on your own; No matter what, you can keep it real. Trust yourself...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?
Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...
-
Ee Mungu Mwenyezi uliyekubali Mwanao Yesu Kristu ateswe mpaka kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zangu naomba uwe nami. Ee Msal...
-
Dodoma. Bunge Maalumu la Katiba linaanza vikao vyake tena leo mjini Dodoma, huku kukiwa na jitihada kubwa za kujaribu kuweka udh...
No comments:
Post a Comment