22 September, 2013

SHANGWE DODOMA: REDD'S MISS TANZANIA 2013

 Personally....Personal Personally......
Shoo ya ufunguzi kwa warembo 30 ilikua matata ile mbayaaaa.....


  MISS Tanzania 2013, Happiness Watimanywa akipunga mkono mara baada ya kuvikwa taji la Redd’s Miss Tanzania 2013 usiku wa Septemba 21, Ndani ya Ukumbi wa Mlimani City na kuwashinda warembo wenzake 29.



top 5 mkao wa kusubiria maswali, kutoka kushoto ni  Happiness Watimanywa (Miss Photogenic), Elizabeth Pretty, Clara Bayo (Miss Sports Women), Lucy Tomeka na Latifa Mohamed.

Hongera kwako Happiness Matimanywa toka Dodoma, really you deserve it. Ulijibu vizuri swali ulilo ulizwa, ulijituma hata ulipokua kambini, mbali na kutwaa taji la Redd's Miss Tanzania 2013, pia Happy anashikilia taji la Miss Photogenic.

Nafasi ya pili ilikwenda kwa mrembo Latifa Mohamed kutoka Kitongoji cha Kigamboni na Kanda ya Temeke na nafasi ya Tatu ikienda kwa Miss Tanzania Sports Woman, Clara Bayo.

 
Ule usemi wa Dua la kuku halimpati mwewe umedhihirika kwani tulisha zoea kila mwaka taji linabaki Dar es Salaam... Sasa hilooooo limeenda zake Dodoma togather with a beautiful red car (Toyota) na kitita cha shilingi milioni 15 za Kitanzania.

Mrembo huyo wa 20 tokea kuanzishwa kwa mashindano haya makubwa zaidi ya urembo Tanzania, ana umri wa miaka 19 tu, huku akiwa tayari na shahada ya usimamizi wa fedha. 

 

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...