Kikao kinachojadili maendeleo ya Chama
cha Demokrasia na Maendeleo Kanda ya ziwa Mashariki (Mara,Simiyu na
Shinyanga) kimemtimua Mbunge wa Maswa Magharibi John Magale Shibuda
baada ya kupiga kura ya kutokuwa na imani naye muda mfupi uliopita jioni
hii.
Shibuda ambaye alihudhuria kikao hichou
kama mbunge wa Kanda hiyo alijikuta akipatwa na zahama hiyo baada ya
mjumbe mmoja kutoa hoja kwa Mwenyekiti wa Kikao hicho kwamba Shibuda
atoke nje.
Mjumbe huyo alisema Shibuda ni mamluki
na kibaraka wa CCM hasa kutokana na matamshi yake kadhaa dhidi ya
Chadema na mwenendo wake usioridhisha ndani ya chama.Aliongeza kwamba
Shibuda alikuwa kwenye kikao hicho kwa lengo maalum la kukusanya habari
na kupeleka CCM.
Hatimaye hoja ya mjumbe huyo iliungwa mkono na wajumbe wote na hatimaye ikapigwa kura ya kutokuwa na imani naye.
Shibuda alikubali kuondoka ndani ya kikao hicho kwa aibu kubwa na hatimaye mkutano umeendelea!
Source:JF
Never afraid to try on your own; No matter what, you can keep it real. Trust yourself...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?
Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...

-
Ee Mungu Mwenyezi uliyekubali Mwanao Yesu Kristu ateswe mpaka kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zangu naomba uwe nami. Ee Msal...
-
Baada ya miaka 13 ya kuwapo katika fani ya sanaa ya maigizo, hakuna shaka kwamba, Ste...
No comments:
Post a Comment