18 November, 2013

WANAO KAMATA WACHAWI NAO WAKAMATWA NA JESHI LA POLISI



Baadhi ya Wataalamu wa kufichua watu wanaojihusisha na vitendo vya ushirikina na uchawi maarufu KAMCHAPE wamejikuta wakiwa kwenye mikono ya dola baada ya kuendesha zoezi la kufichua uchawi katika nyumba kadhaa kwenye vijiji mbalimbali vya manispaa ya Tabora ambapo baadhi ya wananchi walililalamikia zoezi hilo kwa madai kwamba limekuwa likiwadhalilisha baadhi ya watu pamoja na kujenga chuki ambazo huenda zikasababisha madhara makubwa katika jamii.


Hapa ni baada ya kufikishwa kituo kikubwa cha Polisi mjini Tabora kwa amri ya Mkuu wa wilaya ya Tabora Bw.Suleiman Kumchaya ambapo aliwataka kuacha mara moja zoezi hilo la kufichua wachawi

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...