

Hata hivyo, madai ya mitaani yanasema kwamba, watangazaji hao
wamesimamishwa kwa kosa la kukacha sherehe za
maadhimisho ya Miaka 14 ya Clouds FM,
yaliyofanyikia hivi karibuni katika Viwanja vya Mwembeyanga, Temeke,
Dar.

“Ni kweli tumefikia uamuzi wa kuwasimamisha B 12, Diva na Mchomvu baada ya
kukiuka baadhi ya makubaliano baina yao na ofisi, hivyo kusababisha usumbufu
mkubwa ambao ulitulazimu kuingia gharama ambazo hazikutarajiwa.
“Hatutakuwa nao kwa muda usiojulikana, ingawa watu wengi wamekuwa
wakinihoji juu ya hilo lakini watachotakiwa kuelewa ni kwamba hakuna ofisi isiyokuwa
na sheria na taratibu za kuongoza watu wake, sasa hao wamevunja taratibu zetu,”
alisema Ruge bila kufafanua zaidi.
Alipoulizwa ni taratibu zipi watangazaji hao walizovunja alisema:
“Nashindwa kueleza kosa la kila mmoja ila naomba nieleweke kuwa hao watangazaji
kwa sasa tumewasimamisha kwa muda usijulikana wakati tukifikiria cha kufanya.
Muhimu hapo ni kwamba wamekwenda kinyume na tulivyokubaliana.”
|
Credit Musa Mateja
No comments:
Post a Comment