09 January, 2014

MADAM AGNESS SHIJA: “LEO NNAJIVUNIA MATUNDA YAKO”




Mwanzoni wakati nnafungua blog ya JoJoTheFighter;  nakumbuka vizuri sana  ilikua ni assignment tuliyopewa na  lecturer  Agness Shija (kwa sasa ni marehemu ) kupitia course aliyokua akitufundisha  ya International Mass Communication, katika  chuo kishiriki cha Tumaini kilichopo Dar, wakati huo ndio tulikua tumehamishiwa Mikocheni  kwa Warioba baada ya kuhama kutoka Kinondoni.  Kwa sasa nasikia kimehamishwa tena , na sasa kipo Mwenge!


Kiukweli kwa wakati ule mimi na wana chuo wenzangu (sio wote) tuliona kama usumbufu… si unajua tena mambo ya assignment yalivyo na stress hasa linapokuja swala la deadline? Assignment aliyokua ametupa Madam Shija ilikua ni kufungua blog na ku post habari kisha tumtumie link ya blog kwenye email address yake ili aweze kutoa marks! 


Jumapili  ya Tarehe 11 August 2013 asubuhi, nilipatwa na pigo kubwa baada ya kusikia taarifa ya kifo chako! Huko ulipo kama unanisikia, nakupa shukrani toka moyoni. Nakumbuka ucheshi wako, ushauri na juhudi zako zilizonifanya nijifunze mengi kutoka kwako.

Ni miaka mitatu sasa imepita tokea assignment uliyotupa igeuke matunda na kunifanya nipate kipato bila kutumia nguvu kupitia blog! Asante sana Madam.


NITAKUKUMBUKA DAIMA!!!
Mass Comm 3 YEAR 2011 @ Tumaini University DSM 

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...