23 April, 2014

CHADEMA WAENDELEA KUPUKUTIKA

Katibu Mwenezi wa CHADEMA Jiji la Mbeya Lucas Mwampiki amejiuzulu

Katibu Mwenezi wa Chama cha Demokrasia Jiji la Mbeya Lucas MwampikiKatibu Mwenezi wa Chama cha Demokrasia Jiji la Mbeya Lucas Mwampiki amejiuzulu wadhifa huo kuanzia Aprili mwaka huu kutokana na mkanganyiko wa uongozi ndani ya chama hicho.


Mwapiki amesema amechoshwa na malumbano ya mara kwa mara na meza kuu ndani ya chama hicho katika ngazi ya wilaya hivyo kudhoofisha juhudi zake za kukijenga chama hicho.

Aidha Mwampiki amesema viongozi wa chama hicho wamekuwa na malumbano ya mara kwa mara hivyo yeye kama kiongozi hayupo tayari kuona mambo yanavurugika katika chama hicho.

Hata hivyo katika uamuzi aliouchukua Lucas Mwapiki amesema kuwa yeye atabakia kuwa mwanachama wa chama hicho na Diwani wa Kata ya Mwakibete Jijini Mbeya.

Amewataka wanachama wamuelewe hivyo ameona yeye akae pembeni badala ya kuwa na muda mwingi wa kujadili migogoro ambayo haina tija na kuleta mkanganyiko kwa wanachama.

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...