MSANII mahiri wa komedi ambaye pia ni Mwimbaji wa Injili, Emmanuel Mgaya
‘Masanja’ amenaswa akichati kwenye simu wakati viongozi wa dini
wakishusha maombi mazito.
Msanii mahiri wa komedi ambaye pia ni Mwimbaji wa Injili, Emmanuel Mgaya ‘Masanja’ akichati huku maombi yakiendelea
Tukio hilo lililowachefua baadhi ya waumini lilitokea hivi karibuni
katika Uwanja wa Shule ya Msingi Saba Saba, mjini Moro ambapo Masanja
aliyekuwa meza kuu, wakati wenzake wakiongoza sala ya kufungua kongamano
hilo, yeye alikuwa bize na simu.
Kitendo hicho kilidumu kwa dakika kadhaa kisha staa huyo ambaye pia
ana ndoto ya kuwa mchungaji mkubwa nchini, akajiunga na wachungaji
wengine waliokuwa meza kuu kuendelea na sala.
No comments:
Post a Comment