23 June, 2014

TAARIFA NYINGINE KUHUSU KESI YA MUME WA FLORA MBASHA

Hii ni taarifa ambayo ilianzia kusambaa kwenye simu watu kutumiana sauti za sehemu ya kilichotokea kwenye tukio, baadae ikaingia kwenye mitandao mbalimbali zikiwemo blogs na facebook, na sasa ni mpaka kwenye magazeti, Radio na TV.
Taarifa mpya  ni kwamba Emmanuel Mbasha anayekabiliwa na kesi ya kumbaka mdogo wa mke wake, ameachiwa  kwa dhamana baada ya kutimiza masharti katika mahakama ya Wilaya ya Ilala.
Kwenye masharti aliyotimiza Emmanuel ambae ni mume wa mwimbaji Flora Mbasha, ni pamoja na kuwa na wadhamini wawili ambao wote ni wafanyakazi katika taasisi inayotambulika kisheria.
June 17 2014 mbele ya hakimu Willbaforce Rwago wa mahakama hiyo, mwendesha mashtaka wa serikali Nassoro Katuga alidai  kuwa mshatakiwa alitenda kosa hilo Mei 23 mwaka huu eneo la Tabata Kimanga.
Emmanuel Mbasha alifikishwa mahakamani hapo na kukana shitaka la kumbaka msichana mwenye umri wa miaka 17 anaedaiwa kuwa shemeji yake hivyo akarudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.
Mwendesha mashtaka wa serikali alieleza Mahakamani hapo kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na imepangwa kutajwa tena July 17 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...