Hii ni taarifa ambayo ilianzia kusambaa kwenye simu watu kutumiana
sauti za sehemu ya kilichotokea kwenye tukio, baadae ikaingia kwenye
mitandao mbalimbali zikiwemo blogs na facebook, na sasa ni mpaka kwenye
magazeti, Radio na TV.
Taarifa mpya ni kwamba Emmanuel Mbasha anayekabiliwa na kesi
ya kumbaka mdogo wa mke wake, ameachiwa kwa dhamana baada ya
kutimiza masharti katika mahakama ya Wilaya ya Ilala.
Kwenye masharti aliyotimiza Emmanuel ambae ni mume wa mwimbaji Flora
Mbasha, ni pamoja na kuwa na wadhamini wawili ambao wote ni wafanyakazi
katika taasisi inayotambulika kisheria.
June 17 2014 mbele ya hakimu Willbaforce Rwago wa mahakama hiyo,
mwendesha mashtaka wa serikali Nassoro Katuga alidai kuwa mshatakiwa
alitenda kosa hilo Mei 23 mwaka huu eneo la Tabata Kimanga.
Emmanuel Mbasha alifikishwa mahakamani hapo na kukana shitaka la
kumbaka msichana mwenye umri wa miaka 17 anaedaiwa kuwa shemeji yake
hivyo akarudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya
dhamana.
Mwendesha mashtaka wa serikali alieleza Mahakamani hapo kuwa
upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na imepangwa kutajwa tena July 17
mwaka huu.
Never afraid to try on your own; No matter what, you can keep it real. Trust yourself...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?
Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...
-
Ee Mungu Mwenyezi uliyekubali Mwanao Yesu Kristu ateswe mpaka kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zangu naomba uwe nami. Ee Msal...
-
Josephine is passionate, dedicated, reliable, responsible, and hardworking. Team worker and able to face all challenging situations. Can ...
No comments:
Post a Comment