26 August, 2014

UONGOZI WA CHADEMA TANGA MJINI WABWAGA MANYANGA!!

Uongozi wa CHADEMA Tanga mjini wabwaga manyanga, walalamikia ubaguzi na kujiunga ACT
Gazeti ka mwananchi la tarehe 26/8/14 ukurasa wa tano limetoa taarifa ya kujiuzulu kwa Kamati Tendaji ya wilaya ya Tanga mjini.
Wamejiuzulu kwa kukasirishwa na kitendo cha uvunjifu wa katiba ya chama hicho.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari aliyekuwa Katibu wa chadema wa wilaya ya Tanga Khalid Rashid anasema"nimeandikiwa barua ya kusimamishwa uongozi kinyume na taratibu na kupewa tuhuma kumi miongoni mwa hizo ni kupingana na maelekezo ya Kamati kuu kuhusu kumvua nyadhifa aliyekuwa naibu Katibu mkuu Zitto Kabwe"

Khalid anaendelea kusema Mimi na iliyokuwa kamati ya utendaji tumeamua wote kujiunga na chama cha Umoja wa mabadiliko na uwazi (ACT-Tanzania) na tutahakikisha tunakijenga chama mkoa wa Tanga kwa kufanya ziara wilaya zote kuanzi mwezi wa Tisa mwaka huu.
Wajumbe wa Kamati ya utendaji waliojiuzulu na kujiunga na ACT ni:-
Kisua mrami
Hussein baruti
Mohamed kidege
Hassan Maulid
Juma yunusi
Zaina manyeki
Seleman hassan
Mwanaisha kambimbaya
Mohamed sululu.

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...