19 September, 2014

BABA MZAZI APOTEZA MAISHA KWA KUCHAPWA VIBOKO NA WANAE

Jeshi la Polis mkoani Kagera linawashikilia watoto watatu,kwa tuhuma za kumpiga fimbo baba yao mzazi na kumsababishia kifo.
Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polis mkoani Kagera Gilles Muroto,alisema tukio hilo lilitokea mnamo mwezi Septemba 15,katika kijiji cha Mkunyu kata Kikukuru tarafa Mabira wilayani Kyerwa,ambapo watuhumiwa hao ambao hawakutajwa majina yao kutokana na umri wao kuwa chini ya miaka 18,walimuua baba yao mzazi Henry Siliakus(62)kwa kumchapa fimbo hadi akapoteza uhai wake.
 
Muroto alisema watoto hao ambao kati yao mmoja mwenye  umri wa miaka 17 anasoma kidato cha pili katika shule ya Sekondari ya Mkunyu,huku mwenye umri wa miaka 13 ni mwanafunzi wa darasa la nne na mwenye umri wa miaka 11 ni mwanafunzi wa darasa la tatu, wote wakiwa wanasoma katika shule za msingi Mkunyu.
 
Alisema mzazi huyo alikumbwa na mauti hayo kutokana na kupigwa fimbo nyingi kichwani akiwa nyumbani kwake,huku sababu ya awali ya mtafaruku huo uliosababisha kifo ikidaiwa kuwa ni ugomvi wa baba na watoto wake,kwa kile kilichodaiwa marehemu kuwa na tabia ya kuuza chakula cha familia na kuwaacha watoto wakitaabika.
 
Hata hivyo,alisema jeshi hilo bado linaendelea na uchunguzi wa kina juu ya tukio hilo na litawafikisha mahakamani watoto pale taratibu za kisheria juu ya umri wao zitakapokamilika. ITV

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...