Hatimaye Diamond Platnumz amefunguka kuhusu tetesi zinazoendelea kuwa
ameachana na Wema Sepetu na kwamba ana mpango wa kufunga ndoa na
Meninah, Diamond alisema kuwa tetesi hizo zimekuwa zikimhuzunisha kwa
kiasi kikubwa.
“Unajua hizi habari kiukweli zimekuwa zikinihuzunisha sana,” amesema superstar huyo wa muziki wa Bongofleva Tanzania.
“Unajua mie ni mtu mmoja ambaye sipendi kuzunguzia mambo ya rumors,
siju magazeti huwa sipendi kuzungumzia kabisa, kwa kuwa najua kabisa
siwezi kubishana na media kwakuwa media ni kubwa, maana najua utaongea
na huyu na yule siku ya siku utagombana na watu. Ndio maana huwa nakaa
kimya,” ameongeza Diamond anayetusua shows katika nchi mbalimbali ndani
na nje ya Africa kwa sasa.
“Kusema ukweli hili suala limekuwa likiniumiza ‘eti sijui kuna vikao vya
harusi mie nataka kumuoa Meninah’. Kusema ukweli sina mahusiano na
Meninah. Kila mtu anajua mie nina mahusiano na Wema.
“Wema ndo mpenzi wangu, ila wakati mwingine nakuwa naelewa ile inakuwa
ni trick ya kibiashara. Mtu anajua hata nikimuandika vipi ‘Diamond sijui
kafanya nini watu hawawezi kumchukia!
Kwahiyo wanaamua kunitengenezea chuki na maadui kwa watu kuwa nipo na
mwanamke wangu halafu namsaliti” alisema Diamond.
Never afraid to try on your own; No matter what, you can keep it real. Trust yourself...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?
Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...

-
Ee Mungu Mwenyezi uliyekubali Mwanao Yesu Kristu ateswe mpaka kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zangu naomba uwe nami. Ee Msal...
-
Josephine is passionate, dedicated, reliable, responsible, and hardworking. Team worker and able to face all challenging situations. Can ...
No comments:
Post a Comment