Mkuu
wa Rasilimali Watu wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Flora Lupembe
(kulia) akimwagiwa maji baridi na Kaimu Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa
benki hiyo, Rukia Mtingwa katika hafla ya kumwagiana maji baridi
iitwayo ‘Ice Bucket Challenge’ yenye makusudi ya kuchangisha fedha kwa
ajili kusaidia wanawake wanaosumbuliwa na ugonjwa wa fistula. Hafla hiyo
imefanyika jijini Dar es Salaam.
Kaimu
Mhazini Mkuu wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Ivan Tarimo (kushoto)
akimwagiwa maji baridi na mmoja wa mfanyakazi mwenzake katika hafla ya
kumwagiana maji baridi iitwayo ‘Ice Bucket Challenge’ yenye makusudi ya
kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia wanawake wanaosumbuliwa na
ugonjwa wa fistula. Hafla hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam.
Mkuu
wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya NBC, Mussa Jallow (katikati)
naye akimwagiwa maji baridi ili kutimiza azma ya benki hiyo katika
kutafuta fedha ili kusaidia wanawake wanaosumbuliwa na tatizo la ugonjwa
wa fistula nchini.
No comments:
Post a Comment