- HIVI NDIVYOJINSI WACHAWI WANAVYOWEZA KUIBA NYOTA YAKO
Kuna watu wengi sana Duniani wanalia kila wanavyojaribu
kuyakwamua maisha yao inashindikana, lakini hawajui ni kwa nini?! Wapo watu ambao Mungu ameamua kuwanyima mali kwa makusudi
anayoyajua yeye mwenyewe, na kuna watu ambao Mungu hakuwanyima mali
mpango wa Mungu ni kwamba watu hawa wapate mali lakini hawana! Hapa ni
kwamba shetani huamua kuwaonea na kuwadhulumu watu hawa. Unajua kila
mmoja wetu anakitu alichopewa na Mungu ili kuweza kuzikamilisha shughuli
za ulimwengu huu. Ngoja nikupe siri moja kuu sana, kila mwanadamu
anapozaliwa huwa anakitu kinachoitwa nyota, kitu hiki ni ishara au ni
kitambulisho cha mtu huyo katika ulimwengu wa roho ya kuwa yeye kapewa
nini hapa duniani, soma Mathayo 2:1-5. Biblia inasema “Yesu alipozaliwa
zamani za mfalme Herode mamajusi wa mashariki walikwenda kumwona, na
walipofika wakauliza yuko wapi aliyezaliwa mfalme maana tuliiona nyota
yake nasi tumekuja kumsujudia. Ukisikia mamajusi ujue si watu wema. Kasome biblia ya kiingereza imesema ‘Astrologers’ yaani wabashiri au
wanaanga. Pia biblia ya NIV imesema Maggi, yaani washirikina, biblia
nyinge imesema the Meggicians yaani wachawi. Kwa
tafsri hizi moja kwamoja tunatambua kwamba hawa mamajusi kuwa ni
wachawi. Sasa rejea katika kauli yao walipofika kwa Yesu walisema “Yuko
wapi waliyezaliwa mfalme maana tuliiona nyota yake nasi tumekuja
kumsujudia” Nifungue akili yako msomaji wa JoJoTheFighter?? Watu hawa ni wachawi, lakini cha ajabu wanasema wameiona
nyota ya Yesu wakajua ya kuwa aliyezaliwa ni mfalme. Kwa hiyo
tunajifunza kwamba kumbe wachawi wanauwezo wa kutazama katika ulimwengu
wa roho na kutambua kwamba wewe una nyota gani katika maisha yako.
Si kwamba walikosea kwa Yesu kusema
kwamba Yesu ni mfalme, walisema kweli kabisa rejea kauli za Bwana wetu
alipokuwa kwa pilato aliulizwa wewe ndiye mfalme wa wayahudi hakukataa
bali alijibu wewe wasema.pia
akaongeza kusema kwamba ufalme wangu si dunia hii. kwa hiyo ni mfalme.
pia ukirejea katika Isaya 9:6 biblia inasema na uweza wakifalme utakuwa
mabegani mwake; Hivyo basi wachawi wakishatazama katika ulimwengu wa
roho na kuona nyota yako kuwa ni ya kifalme kama ya Yesu au labda nyota
yako ni Biashara, au Elimu, au Ajira,nk. wanachokifanya ni kwamba
wanaiba ile nyota na kuiweka kwa mtu mwingine au wakaiacha tu.
Kuna dalili za kutambua nyota yako ni ipi
hasa ni rahisi sana kutambua nyota ya mtoto mdogo. kwa mfano: mtoto
akiwa na nyota ya uongozi,utambua hivi watafute wanapokuwa wanacheza
watoto wengi kwa pamoja, kisha angalia vizuri kaa utulie usipige kelele
kisha uangalie vizuri ni lazima atakuwepo mtoto atakayewadhibiti wenzake
na kuwalazimisha kufanya anavyotaka yeye na lazima watafanya, kwamfano
anawezakusema nyamazeni na wote kweli wakanyamaza, au twendeni na wote
kweli wakamfuata.
Pia dalili za kutambua Nyota iliyoibiwa
ni hizi, kwa mfano mtoto alikuwa anafanya vizuri kabisa darasani lakini
sasa hivi anazidi kudidimia wala hapendi kusoma, ukiona hivyo ujue
tayari wameshachukua wanjanja! pia kwa mtu mzima unaweza kukuta kwamba
unaandaa mipango lakini haitimii mipango yako. Unapanga mwaka huu lazima
nitafungua Duka lakini utashangaa linazuka tatizo hutafungua hilo duka
mpaka mwaka utaisha. Au unaandaa mpango mzuri kabisa lakini utashangaa
unamwona mwenzako tayari ameshaanzisha mpango uleule kama ulivyokuwa
unapanga. au kama ni biashara utaona mwingine kaanzisha vilevile kama
ulivyokuwa unafikilia hapo ujue Nyota yako inatumiwa na mwingine. Unajua
nyota hizi huambatana na mawazo yako. Jinsi mawazo yako yalivyo ndivyo
na nyota yako ilivyo hawezi mtu akaitumia nyota yako pasipo mawazo
yako. Utajikuta kwamba wakati mwingine unapoteza fahamu kama hujielewi
vizuri vile. Hapo ujue kuna kitu.

No comments:
Post a Comment