22 November, 2014

WATOTO WAWILI WA KIMASAI WAMPIGA FIMBO MKULIMA HADI AKAFA HUKO TANGA


Jeshi la Polisi Mkoani Tanga limewatia mbaroni watoto wawili wajamii ya wafugaji wa kimasai kwa tuhuma za kumuua kwa kumpiga na fimbo kichwani mkulima Nassor Mwinyiheri mwenye miaka45 mkazi wa Wilaya ya Handeni.
Watuhumiwa hao wenye umri wa miaka14 na mwingine 12 wakazi wa Wilaya ya Handeni wanadaiwa kumuua mkulima huyo kwa kumpiga na fimbo kichwani wakati akiwazuia kuingiza mifugo yao kwenye shamba lake lililopo kijiji cha Kwamagome.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Frasser Kashai alisema watuhumiwa hao walikamatwa kufuatia msako mkali uliofanywa na wanakijiji wakisaidia na polisi baada ya kutokea mauaji hayo.
Vijana hao wanaatarajiwa kufikishwa mahakamani hivi karibuni baada ya upelelezi kukamilika.

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...