
Jeshi la Polisi Mkoani Tanga limewatia mbaroni watoto wawili wajamii
ya wafugaji wa kimasai kwa tuhuma za kumuua kwa kumpiga na fimbo
kichwani mkulima Nassor Mwinyiheri mwenye miaka45 mkazi wa Wilaya ya
Handeni.
Watuhumiwa hao wenye umri wa miaka14 na mwingine 12 wakazi wa Wilaya
ya Handeni wanadaiwa kumuua mkulima huyo kwa kumpiga na fimbo kichwani
wakati akiwazuia kuingiza mifugo yao kwenye shamba lake lililopo kijiji
cha Kwamagome.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Frasser Kashai alisema watuhumiwa hao
walikamatwa kufuatia msako mkali uliofanywa na wanakijiji wakisaidia na
polisi baada ya kutokea mauaji hayo.
Vijana hao wanaatarajiwa kufikishwa mahakamani hivi karibuni baada ya upelelezi kukamilika.
No comments:
Post a Comment