01 December, 2014

DIAMOND PLATNUMZ ALIVYOFANYA KWELI TUZO ZA CHANNEL O NCHINI AFRIKA KUSINI

Mrembo Zari anayedaiwa kuchukua nafasi ya Wema Sepetu akiwa ameshika tuzo za Diamond.
Diamond Platnumz akipozi baada ya kutwaa tuzo tatu za Channel O jana usiku nchini Afrika Kusini.

Diamond Platnumz akiongea machache baada ya ushindi huo wa kishindo.
Diamond katika pozi na wadau.
Diamond katika pozi na wadau pamoja na mama yake mzazi, Sandra (wa pili kulia).
Diamond (katikati) akiwa na management yake. Kulia ni Said Fella na Babu Tale (kushoto).
Mama mzaa chema, Sanura 'Sandra' Kassim katika pozi.
Kutoka kushoto ni Mama mzazi wa Diamond 'Sandra', Diamond na Zari katika picha ya pamoja.
MSANII Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ ametwaa tuzo tatu za Channel O jana usiku nchini Afrika Kusini. Tuzo hizo ni; Most Gifted new comer, Most Gifted Afropop na Most Gifted East kupitia wimbo wake wa Number One.
Kupitia ukirasa wake wa Facebook Diamond amewashuru sana mashabiki wa wote walio msupport.
"Kiu kweli, haikuwa rahisi kabisa.. lakini kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu na support kubwa mliyonipa iliwezesha Bongo Flavour yetu kuandika historia mpya kwenye ramani ya muziki wa Afrika...Hii inaonyesha ni jinsi gani umoja ni nguvu na pia jinsi gani muziki wetu ukisupportiwa na kupewa kipaumbele unaweza kufika mbali zaidi... Shukrani sana kwa @channeloafrica @channelotv kwa kuniona na kuthamini kipaji changu, My Family, Management, Media zote zilizokuwa zikinisupport, Watangazaji, Wasanii, Wadau na bila kuwasahau wapendwa wangu" - Ameandika Diamond.
Askari wa JKT akutwa mferejini akiwa kalewa chakari .....Pombe Ilipozidi alianza kujisaidia ndani ya basi 12/01/2014 12:01:00 AM Shaban R Dege 0 KITAIFA Katika hali isiyotegemewa askari mmoja wa jeshi la kujenga Taifa (JKT) anayesadikika kuwa ni wa kambi ya Mafinga wilaya ya Mufindi mkoani Iringa usiku wa jana amenusurika kuvuliwa nguo za jeshi hadharani baada ya kukutwa amelewa chakari na kulala katika mfereji wa maji machafu eneo la nje ya stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani mjini Iringa Tukio hilo lilitokea muda wa saa 2 usiku baada ya wasamaria wema kumshusha askari huyo kutoka katika basi la Mgumba ambalo alikuwa amepanda kutoka Mafinga kuja mjini Iringa. Akisimulia kisa na mkasa wa askari huyo kulewa chakali kiasi cha kushindwa kujitambua mmoja kati ya wasamaria wema aliyejitolea kumshusha katika basi hilo alisema kuwa askari huyo alipanda basi hilo Mafinga huku akiwa amelewa na wakati wote wa safari alionekana akinywa pombe kali kiasi cha kushindwa kujimudu na kuanza kutapika na kujisaidia haja ndogo ndani ya basi hilo. Hata hivyo alisema baada ya kufika stendi ilikuwa ni vigumu kujitambua hivyo kupoteza fahamu na kulazimika kumpa msaada na kumzimua kwa maji kabla ya kupata fahamu kiasi na kujificha chini ya mfereji wa maji machafu . Alisema kuwa mara baada ya kujitambua kiasi aliweza kutoa namba ya ndugu yake ambae ni askari wa FFU mjini Iringa aliyefika kumnusuru kuvuliwa nguo na kiongozi wake aliyefika eneo hilo na kumtukana akilishushia heshima jeshi kwa ulevi uliopitiliza "Umelidhalilisha sana jeshi kwa askari kulewa hivi ukiwa katika sare, sasa nataka kukuvua sare kisha nakupeleka kulala polisi kabla ya kesho kukuchukulia hatua zaidi " alisikika akisema kiongozi huyo ambae jina wala cheo chake hakukitaja. Maamuzi hayo ya kiongozi wake yaliwafanya mashuhuda kumuangukia na kumwomba amsamehe kwani bado ni kijana mdogo sana maombi ambayo aliyakubali na ndugu zake kumpakiza katika Taxi na kumpeleka eneo la Kihesa.

Make Money at : http://bit.ly/copy_win

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...