10 December, 2014

HII NDO SARAFU MPYA YA TSH. 500/= ILIYOANZA KUTUMIKA HIVI KARIBUNI

Sarafu mpya ya Tsh. 500/= inayotumika sasa
 
Baada ya kuonekana noti ya shilingi 500 ina mzunguko mkubwa wa matumizi na inachakaa kwa haraka huku kiwango chake cha kuhimili mizunguko ni miezi sita, Benki kuu ya Tanzania (BOT) imekubadili kubadili noti hiyo na kuifanya sarafu.
Sarafu hiyo ya 500 imesha anza kutumika ikienda sambamba na kipindi cha mwaka huu wa fedha ambapo inaarifiwa sarafu hii inatarajiwa kudumu kwenye mzunguko kwa zaidi ya miaka 20 na kubaki na ubora wake uleule, yani ni imara kuliko noti.
Noti ya 500 iliyokua ikitumika awali
Afisa mkuu wa benki kitengo cha idara kurugenzi za kibenki Patrick Fata amesema “Tunafanya hivi kwasababu noti ya 500 inachakaa haraka kulinganisha na mzunguko wake na kuwafikia watu wengi pia huchakaa haraka kutokana na mzunguko wa kushikwa na watu wanaofikia mpaka milioni moja kwa siku, hiyo ni idadi kubwa kuliko ya wanaoshika noti ya elfu 10 kwa siku’

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...