01 December, 2014

JIDE AANIKA KISA CHA KUMMWAGA GARDNER

Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ akiwa na Garder.Stori: Gladness Mallya
Funguka! Kwa mara ya kwanza, staa wa muziki wa Bongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ ameanika kisa cha kummwaga mumewe, Gardner Gabriel Habash ‘Kaptein’ akieleza mateso aliyokutana nayo kwenye ndoa yao
.
Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ akipozi.
Akizungumza na Kituo cha Radio Times FM cha jijini Dar, wikiendi iliyopita, Jide alifunguka kuwa yeye ndiye aliyeamua kummwaga Gardner.
Katika mahojiano hayo, Jide alisema kwamba alikuwa kwenye uhusiano na mtu aliyekuwa akimpiga mara kwa mara licha ya kutomtaja moja kwa moja kuwa ni Gardner lakini alisema alikuwa akiteswa (hakuna mwanaume mwingine zaidi ya Gardner)
About Contact More Menu December 1, 201422:45:15 twitter facebook google rss linkedin dribbble pinterest SHEBBY D BLOG NI BLOG INAYOJIUSISHA NA JAMII YOTE KWA UJUMLA Home KITAIFA KIMATAIFA SIASA ENTERTAINMENT AUDIO VIDEO KISURA SOKA facebook contact Hisia za Mwananchi Home » KITAIFA » SIASA » Escrow yazamisha watatu Urais 2015 Escrow yazamisha watatu Urais 2015 12/01/2014 10:12:00 AM Shaban R Dege 0 KITAIFA, SIASA KASHFA ya uchotwaji wa zaidi ya Sh bilioni 300 kwenye akaunti ya Tegeta Escrow, imewachafua viongozi watatu ambao walishaanza harakati za kuusaka urais kwa mwaka 2015. Baadhi ya viongozi hao ni pamoja na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka. Kwa upande wa Pinda, ripoti ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iliyowasilishwa bungeni, ilionyesha kiongozi huyo wa shughuli za Serikali bungeni alilidanganya Bunge kwa matamshi yake. Mara kadhaa Pinda alisikika akiueleza umma kuwa fedha hizo hazikuwa za umma bali mali ya Kampuni ya Kuzalisha Umeme ya IPTL. Katika maazimio ya PAC, Pinda alitakiwa pia kuwajibika kutokana na kushindwa kusimamia Serikali kwani katika hatua zote za kutolewa kwa fedha hizo, alikuwa akijulishwa. Pinda ambaye alitangaza kuanza harakati za urais kimya kimya, akiwa jijini London, Uingereza alipohojiwa na Kituo cha Televisheni cha BBC, alijikuta kwenye wakati mgumu pale Bunge lilipopitisha azimio la kumpeleka kwa mamlaka ya uteuzi kabla baadae jina lake kuondolewa. Hali hiyo ilijitokeza pale Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe alipolishauri Bunge kupeleka majina ya watu wote waliotakiwa kuchukuliwa hatua kwa mamlaka zao za uteuzi ili hatua zaidi zichukuliwe. Baada ya kauli hiyo ya Zitto, Spika wa Bunge Anne Makinda alilihoji Bunge na kwa sauti moja likakubali kabla ya Mbunge wa Simanjiro, Ole Sendeka kusimama na kuomba mwongozo wa Spika ambaye baadaye alitengua uamuzi wake. Akizungumza na Mtanzania, Zitto alisema jina la Pinda kupelekwa kwa rais ingetosha kuonyesha Bunge halina imani naye, hivyo mamlaka yake hiyo ya uteuzi ingebidi itengue nafasi ya kiongozi huyo wa shughuli za Serikali bungeni. Alisema pia kamati yake ilikubali kuondoa jina la Pinda kwenye orodha ya vigogo waliopaswa kushughulikiwa baada ya mazungumzo kati ya wabunge wa upinzani na wale wa CCM. Kutokana na hali hiyo, Pinda ambaye anajulikana zaidi kama ‘mtoto wa mkulima’, harakati zake za kwenda Ikulu zimetiwa doa kwani mwanzo alihesabika kuwa ni kati ya wagombea wasio na kashfa. Kwa upande wake, Ngeleja ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini, anadaiwa kupewa Sh milioni 40.4 kutoka kwenye akaunti ya Escrow huku Profesa Tibaijuka ambaye ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, akidaiwa kupewa Sh bilioni 1.6. Viongozi wote hao wawili ambao hawajawahi kutangaza rasmi kuwania urais mbali na majina yao kutajwa kwenye orodha hiyo, Bunge limeazimia wachukuliwe hatua. Kwa upande wa Profesa Tibaijuka, rais ametakiwa kumvua wadhifa wa uwaziri huku Ngeleja ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala, spika akishauriwa kumchukulia hatua ya kumvua wadhifa huo. Akichangia bungeni, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu, Steven Wasira, aliwataka wote wanaotumia suala la ripoti ya PAC kwa vigezo vya kuwaondoa wenzao katika mbio za urais hawastahili kupewa nafasi hiyo. “Wanaotaka urais kama wapo ni pamoja na mimi, ambao wanaona mbinu ni kuwaondoa wengine kwa nguvu, hao hawafai kupewa urais wa nchi hii. Urais ni lazima ushindaniwe kwa haki na vyama vyote vipewe nafasi ya kushiriki. Kama unataka urais ushindani uwe kwa njia sahihi,” alisema. Alisema ni bora kuwa maskini anayeheshimika kuliko kukubali kuwa tajiri anayedharauliwa na kutukanwa kutokana na mapato yasiyokuwa halali. Wasira alieleza kwa kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imesema baadhi ya watu walikwenda kuchukua fedha wakiwa na magunia, mifuko ya sandarusi, rumbesa na maboksi katika moja ya benki, ni vyema uchunguzi ukifanyika ili kuwatambua watu hao na hatua zaidi zichukuliwe. “Ni lazima tufuatilie na vyombo vyetu vya sheria vituambie ni kina nani hao, vinginevyo hatuna nchi. Tukubali hawa watu wabebe mizigo yao, hakuna CCM ya wezi, ila kuna wezi ndani ya CCM, hivyo wezi ni lazima wabebe mizigo yao,” alisema. Alisisitiza kwamba ripoti hiyo ya PAC inatakiwa kuheshimiwa na kwamba hakuna mtu mwenye mamlaka ya kuihoji uhalali wake kwa kuwa inatokana na kamati maalumu inayotambuliwa na Bunge iliyokusanya taarifa kutoka kwa vyombo vinavyoaminika vya Serikali, ambavyo ni Takukuru na CAG. Credit:Mtanzania Share to: Next This is the most recent post. Previous Kama hujasoma Magazeti ya Leo Desemba 01 nimekuwekea hapa zile story kubwa zote. Related Posts Kama hujasoma Magazeti ya Leo Desemba 01 nimekuwekea hapa zile story kubwa zote.Kama hujasoma Magazeti ya Leo Desemba 01 nimekuwekea hapa zile story kubwa zote.Dec 01, 2014 Taarifa rasmi kutoka Ikulu kuhusu mabadiliko kwenye nafasi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali, CAGTaarifa rasmi kutoka Ikulu kuhusu mabadiliko kwenye nafasi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali, CAGDec 01, 2014 Askari wa JKT akutwa mferejini akiwa kalewa chakari .....Pombe Ilipozidi alianza kujisaidia ndani ya basiAskari wa JKT akutwa mferejini akiwa kalewa chakari .....Pombe Ilipozidi alianza kujisaidia ndani ya basiDec 01, 2014 Watendaji 17 Waswekwa Rumande kwa Kushindwa Kusimamia Agizo la Rais Kikwete kuhusu Ujenzi wa MaabaraWatendaji 17 Waswekwa Rumande kwa Kushindwa Kusimamia Agizo la Rais Kikwete kuhusu Ujenzi wa MaabaraNov 27, 2014 Baada ya Ishu ya Escrow, haya ni Majibu Mawili ya Waziri Mkuu Pinda ikiwemo KujiuzuluBaada ya Ishu ya Escrow, haya ni Majibu Mawili ya Waziri Mkuu Pinda ikiwemo KujiuzuluNov 27, 2014 #Exclusive Staa mwingine wa Tanzania alietangaza kugombea Ubunge 2015.#Exclusive Staa mwingine wa Tanzania alietangaza kugombea Ubunge 2015.Nov 19, 2014 Kinana na Dr. Slaa kesho watashiriki katika Mjadala wa Rais wa Tanzania anayetakiwa 2015Kinana na Dr. Slaa kesho watashiriki katika Mjadala wa Rais wa Tanzania anayetakiwa 2015Nov 11, 2014 Rais Kikwete Aomba Yasimkute ya Jaji Warioba.....Polisi watoa tamko, CUF Waapa kulinda midahalo ya Jaji Warioba!Rais Kikwete Aomba Yasimkute ya Jaji Warioba.....Polisi watoa tamko, CUF Waapa kulinda midahalo ya Jaji Warioba!Nov 04, 2014 Post a Comment toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment Emoticon Live streaming video by Ustream Blog Rafiki JOHVENTURE MUSIC Official Video | Ommy Dimpoz -Tupogo Remix | Download - 3 days ago Total Pageviews 349874 Populars Comments Archive widgeo.net widgets SHEBBY D BLOG © 2013. All Rights Reserved. Share on Hisia za Mwananchi. Powered by Hisia Top SOMA HABARI KEM KEM KUPITIA BLOG YAKO PENDWA YA HISIA ZA MWANANCHI HAPA X FacebookTwitterEmailPrintGmailStumbleUponFavoritesMore... (294) Sign In AddThisPrivacy

Make Money at : http://bit.ly/copy_win

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...