Katika
kukua kwangu nimejifunza matumizi ya rasilimali na kuset priorities
(vipaumbele). Kama nina laki moja mfukoni, halafu nikawa na matumizi
yanayohitaji zaidi ya hiyo hela nitaangalia lile la muhimu ndio nianze
nalo. Yani kama
umepanga kununua radio halafu mama yako akaugua, ukaacha kumpeleka mama
yako hospitali ili pesa ukanunulie "sub woofer", wewe ni goigoi.!
One
of the cardinal principles of Economics is Opportunity Cost. Do the
fast thing first, and those which can wait let them wait. Ni
mwendawazimu pekee anayeweza kununua Jeans mpya ya laki moja wakati
hajalipa kodi ya nyumba. Ukiwa na akili timamu utafanya yale ya muhimu
kwanza kwa rasilimali kidogo uliyonayo kabla ya kufikiria kufanya anasa.
Nasema
haya kwa sababu kuna kituko cha mwaka kimetokea leo. Kituko cha aibu
kufanywa na mtu mkubwa kama huyo aliyefanya. Lakini kwa kuwa alishazoea
kufanya vituko vingi sikustajaabu kusikia na leo kafanya tena kituko.
Kituko
chenyewe ni hiki. Leo "mkuu wa kaya" kateua wabunge wawili kwa mujibu
wa Mamlaka aliyopewa kikatiba. Katika tangazo la Ikulu lililotolewa na
Ndg.Premi Kibanga (Afisa Habari msaidizi) inasema "mkuu wa kaya" kateua
wabunge hao ili kutimiza idadi ya wabunge 10 wanaotakiwa kikatiba.
Kwa
lugha nyingine ni kuwa hakuna sababu yoyote ya msingi ya uteuzi wao
zaidi ya kutimiza matakwa ya kikatiba ya kufikisha wabunge 10. Yani
hakuna impact yoyote hao wabunge wanayoweza kuleta bungeni kwa kipindi
hiki kilichobaki, wala hakuna kazi yoyote maalumu iliyochochea uteuzi
wao, itz just that "mkuu wa kaya" amejisikia kumalizia nafasi zake 10
alizopewa.
Swali
nililojiuliza ni "hivi ni lazima wafike 10?" Hivi asingewateua kuna
mahali popote angeshtakiwa kwa kushindwa kutumia haki yake kikatiba to
the maximum? (Hapa naomba ufafanuzi wa kisheria kwa wale waliosoma
Constitutional Law).
Kama
sivyo, uteuzi huu una mantiki gani? Bora akina Muhongo na Saada Mkuya
au Makame Mbarawa ambao waliteuliwa Ubunge wa ghafla ili wapewe kazi
maalumu ya Uwaziri na Unaibu Waziri. Sasa hawa walioteuliwa leo ni kwa
mantiki gani?? Tena ukizingatia kuwa imebaki miezi mitano tu bunge
kuvunjwa.
Hebu
tujaribu kufanya hesabu ndogo za kugawanya na kuzidisha za darasa la
tano. Ni hivi, wabunge wawili walioteuliwa watalipwa mishahara ya miezi
mitano bure maana hatutegemei jipya watakalolifanya huko bungeni.
Mshahara kwa mbunge mmoja ni Mil.11 mara miezi mitano watakayofanya kazi
ni jumla ya Sh.Mil 55 kwa kila mmoja. Kwa wote wawili ni Mil.110.
Wabunge
hawa walioteuliwa leo watalipwa kiinua mgongo kwa viwango vya wabunge
wa kawaida Sh.Mil.90 kila mmoja ifikapo tar.31 mwezi July mwaka huu. Kwa
wote wawili ni Mil.180.
Taarifa
ya Ikulu inasema uteuzi wao unaanza tarehe 20, hivyo basi kuanzia
tar.21 wataanza kulipwa posho za vikao vya bunge kwa siku 10 zilizobakia
kwenye bunge hili linaloendelea. Posho ya siku moja ni Sh.330,000/= kwa
siku kumi ni Mil.3 na laki 3.
Kwenye
bunge la bajeti Watalipwa posho ya 330,000/= kwa siku. Bunge hilo
litatumia jumla ya siku 60. Hivyo mbunge mmoja atalipwa Mil.19 na laki
8, kwa muda wote wa bunge la bajeti. Kwa wote wawili watalipwa mil.39 na
laki 6.
Wabunge
hawa "watakopeshwa" magari ya kifahari ya kutembelea. Yani kama walikua
wakitumia usafiri wa umma, kuanzia tar.20 March wameambiwa stop.
Watapanda Mashangingi yanayokadiriwa kugharimu Mil.120 kwa moja, kwa
wote wawili ni Mil.240.
Kwa
ujumla makadirio ya gharama zote za wabunge hawa wawili kwa miezi
mitano tu watakayofanya kazi watatumia jumla ya Shilingi Milioni 573 na
laki 2.
Pesa
hizi zinatosha kulipia mikopo ya elimu ya juu kwa semister moja kwa
wanafunzi wote wa mwaka wa kwanza Chuo kikuu cha St.Augustine, au Chuo
Kikuu Dodoma kwa wanafunzi wanaosoma Social Science.
Pia
pesa hizi zingeweza kujenga maabara za kisasa katika shule 12 Tanzania.
Zingeweza kulipa mishahara ya waalimu (daraja la pili) 1,432 wa shule
mbalimbali za sekondari nchini. Pia fedha hizi zingeweza kutolewa kama
mkopo kwa vijana wanaohitimu vyuo vya Elimu ya juu nchini na kukosa
ajira. Jumla ya vijana 573 wangenufaika kwa mkopo wa Mil.1 kila mmoja.
Lakini
cha ajabu pesa zote hizi zitatumiwa na wabunge wawili tu tena kwa
kipindi cha miezi mitano tu, with no expectation of return. Hatutegemei
wabunge hawa watafanya lolote jipya huko bungeni litakalogharimu hizo
Mil.573 watakazotumia.
Kwa
lugha rahisi ni kuwa hatutegemei output ya wabunge hawa izidi input.
Hakuna mbunge yeyote atakayeweza kutoa hoja zitakazo-value hizo Mil.573
watakazotumia, hata wakisaidiwa na huyo aliyewateua.
Sasa
nimejiuliza, hivi katika mazingira haya ambayo hatuna rasilimali za
kutosha kulinganisha na mahitaji tuliyonayo, je kulikua na ulazima
wowote wa kuteua wabunge hao?
Tunahitaji
pesa za kujenga maabara, kujenga shule, kulipia wanafunzi wa vyuo vya
elimu ya juu mikopo, kulipa mishahara, kununua madawa etc. Lakini
tumeacha vyote hivyo tumetoa kipaumbele kwa wabunge tena wa kuteuliwa.
Yani
mkuu wa kaya ameona heri wagonjwa wafe kwa kukosa dawa, wadogo zetu
wateseke vyuoni kwa kukosa mikopo just for the expense of two appointed
Mp's
Never afraid to try on your own; No matter what, you can keep it real. Trust yourself...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?
Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhpTo4YV7Oox_BVlRsooBaHFJreydnAhg3m50m_mGMwYjIKhkSy2I-0rErStBFcxsPYwCkQJaczXQLKQ5zGlZEaQxNsuuOisHrgroUOvPckYInirjwF1zOXw-MD_2z7d8bzIW6Fl7mX0u8QtMRuafCU_STytqBGuUCEe7iB3QkG0IT9PgpCHyXDLNm_rC5T/s320/Horace-Mann.webp)
-
Ee Mungu Mwenyezi uliyekubali Mwanao Yesu Kristu ateswe mpaka kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zangu naomba uwe nami. Ee Msal...
-
Josephine is passionate, dedicated, reliable, responsible, and hardworking. Team worker and able to face all challenging situations. Can ...
No comments:
Post a Comment