18 November, 2023

AFISA WA POLISI WA TANZANIA ALIKODI RAFIKI ILI AMPE MKE WAKE MIMBA, AMFIKISHA MAHAKAMANI KWA KUSHINDWA KUMPA MIMBA BAADA YA KUJARARIBU MARA 77

Jijini Dar-es-Salaam, Mahakama ya Tanzania lazima iamue juu ya nia ya heshima katika kesi ambapo mwanamume alimwajiri jirani yake ili kumpa ujauzito mkewe.

 

Inaonekana kwamba Darius Makambako 50 akiwa na mke wake Precious 45, walitaka sana kupata mtoto, lakini daktari bingwa alikuwa amewaambia wanandoa hao kuwa mume alikuwa TASA. Hakukuwa na shaka, wenzi hao walikuwa wamechoka kuwa katika ndoa ya miaka 23 bila mtoto.

 

Kwa hiyo Makambako, askari wa Jeshi la Polisi (Idara ya Trafiki), baada ya kushurutishwa na mkewe, aliajiri jirani yake Evans Mastano, 52, afisa mwenza wa polisi katika jiji la kibiashara la Dar-es-Salaam kumpa ujauzito mke wake.

 

Kwa kuwa Evans alikuwa tayari ameoa na ni baba wa mabinti wawili warembo, na pia kwamba alifanana sana na Darius kindakindaki, mpango huo ulionekana kuwa mzuri kwa wanandoa hao wa familia mbili lakini bila kumshirikisha mke wa Evans.

 

Makambako alimlipa Mastano Shilingi 2,000,000 za Kitanzania kwa kazi hiyo ambayo angeshiriki tendo la ndoa na mkewe kwa jioni tatu kwa wiki kwa miezi 10 ijayo ya 2016.

 

Evans alijaribu sana, jumla ya mara 77 kumpa ujauzito mke wa rafiki yake Precious, lakini alishindwa kabisa kufanikiwa.

 

Ripoti zinasema Precious, ambaye kikazi ni muuguzi katika zahanati ya kibinafsi aliamua kuchukua likizo ya miezi mitatu (Machi hadi Juni 2016) ili kutenga muda wake wa kulala na rafiki mkubwa wa mumewe na jirani ili kupata mtoto wake wa kwanza, lakini mwanamume huyo alishindwa kumpa mimba licha ya mume kuwaacha kitandani siku nzima mara nyingi.

 

Na Precious aliposhindwa kupata ujauzito kwa miezi 10, hata hivyo, Makambako hakuelewa na kusisitiza kwamba Evans afanyiwe uchunguzi wa kimatibabu, ambao alifanya Januari 2017.

 

Uchunguzi wa daktari

Ulionyesha kwamba Evans Mastano pia alikuwa TASA matokeo ambayo yalimshtua kila mtu isipokuwa mkewe (Evans), ambaye alilazimika kukiri kwamba Evans hakuwa baba halisi wa watoto wake wawili, bali walikuwa wa binamu yake, Edward.

 

" _Nililazimika kulala kwa siri na Edward, binamu yake wa kwanza, kupata watoto hawa wawili baada ya kugundua kuwa mume wangu hangeweza kunipa ujauzito kwa miaka miwili",_ Angela aliambia _Dar-es-Salaam Today News._

 

Sasa Makamboko anamshtaki Evans kwa ukiukwaji wa masharti ya mkataba katika jitihada za kurejesha pesa zake, lakini Evans anakataa kwa sababu alisema hakumhakikishia kupata mimba, lakini tu kwamba aliahidi kujitahidi na angefanya juhudi za uaminifu.

 

 *SWALI* : 

 

1. Je. Makambako ana haki ya kudai arudishiwe pesa yake? 

2. Nini itakuwa hatma ya ndoa kati ya Evans na mkewe Anjela?

 

Chanzo: *DAR-ES-SALAAM LEO.*


No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...