Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete aliwasamehe wafungwa 3,814 siku ya Jumapili (tarehe 9 Disemba) kwa heshima ya miaka 51 ya uhuru wa Tanzania, Waziri wa Mambo ya Ndani Emmanuel Nchimbi alitangaza.
"Serikali inatumai kuwa wale waliochiwa huru wanakwenda kujiunga na
jamii katika ujenzi wa taifa na kuepuka uhalifu ili wasirejee tena
gerezani," Nchimbi alisema katika taarifa.
Kikwete aliwasamehe wafungwa wanaotumikia vifungo vya miaka mitano na
tayari walishatumikia robo ya adhabu ya zao, gazeti la Daily News la
Tanzania liliripoti. Wafungwa wanaoteseka na maradhi ya muda mrefu,
ikiwa ni pamoja na VVU/UKIMWI, kifua kikuu na saratani pia walisamehewa,
wakisubri kuthibitishwa na jopo la taalamu wa afya. Wengine
walioachiliwa ni pamoja na wanawake wanaonyonyesha, watu wa zaidi ya
umri wa miaka 70, watu wenye ulemavu wa kimwili au kiakili.
Wafungwa wanaotumikia vifungo vya muda mrefu kwa makosa makubwa,
ikiwa ni pamoja na biashara ya madawa ya kulevya, wizi wa magari au
uharibifu wa miundombinu, au kosa lolote ambalo linachukua kifungo cha
maisha, hawakusamehewa.
Kikwete pia aliwatunukia nishani watumishi bora wa umma 40 kwa kazi
zao za mfano kwa taifa, ikiwa ni pamoja Nishani 11 za Ushujaa kwa
wanajeshi walioiokoa meli iliyokuwa imetekwa na maharamia katika Ziwa
Tanganyika.
Never afraid to try on your own; No matter what, you can keep it real. Trust yourself...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?
Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...

-
Ee Mungu Mwenyezi uliyekubali Mwanao Yesu Kristu ateswe mpaka kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zangu naomba uwe nami. Ee Msal...
-
Baada ya miaka 13 ya kuwapo katika fani ya sanaa ya maigizo, hakuna shaka kwamba, Ste...
No comments:
Post a Comment