Mkuu wa Wilaya kushoto akipokea maelekezo kutoka kwa mmoja wa wafanyakazio wa kampuni ya maji Iringa
Handaki la ajabu limeonekana katika eneo la kata ya kitanzini mtaa wa sokoni Katika tukio hilo lililokuwa gumzo kubwa katika eneo hilo huku kila mmoja akisema lake.
Handaki hilo ambalo lilionekana jana na wachimbaji wa mitaro wa JR
wanaoshuhulika na uwekwaji wa mabomba mapya ya maji safi wanaeleza
katika kuchimba ndipo walipokutana na chemba hiyo ikiwa imefunikwa na
kudhani kuwa inatumika kama shimo la choo ya nje lakini haikuwa hivyo
maana lilikuwa wazi limejengewa na hakuna dalili ya kutumika kama choo.
Akizungumza mmoja wa wananchi aliyeingia katika handaki hilo Abdukareem
ameeleza kuwa yeye ni mkazi wa eneo hilo na alipopata taarifa alifika
akiwa na mwenzake aliyefahamika kwa jina la Salehe na kukubaliana
kuingia ndani ili kufahamu kilichopo.
Ameeleza kutokana na shimo hilo kuwa refu walitafuta ngazi lakini
hawakufanikiwa kwani ngazi hiyo ilikuwa pana na kuamua kutafuta fimbo
kubwa ya muanzi na kamba na ndipo walipofanikiwa kuingia ndani.
Anazidi kueleza kuwa walipofika ndani walikuta chumba ambacho ni kama
futi tatu na kuona vidirisha vidogo kwa mbele huku bado kukiwa
kumejengewa kwa zege na kubainisha kuna muendelezo wa chemba nyingine
ambapo hawakuweza kuendelea kutokana na kuzibwa.
Mkuu wa wilaya ya Iringa Dkt Leticia Warioba akafika katika eneo la
tukio huku akiwa na wafanyakazi wa Kampuni ya JR pamoja na afisa wa
usalama ambao waliishia kuangalia njia hiyo pasipo kuingia ndani ya
handaki hilo.
Wengi wa wakazi waliofika katika eneo hilo hawakusita kueleza hisia zao
huku wengine wakieleza labda ni mahandaki yaliyokuwa yakitumiwa na
Wajerumani enzi za ukoloni, huku wengine wakieleza labda handaki hilo
limekuwa likitumiwa na majambazi kama sehemu za kujificha na kuhifadhia
mali walizoiba japo hapakuonekana na mali aina yeyote.
No comments:
Post a Comment