Never afraid to try on your own; No matter what, you can keep it real. Trust yourself...
20 May, 2014
SERIKALI IANGALIE UDHALILISHAJI UNAOFANYWA NA CLOUDSTV KUPITIA KIPINDI CHA BIBI BOMBA
Bibi mmoja aliulizwa kama aliwahi kula mboga inayoitwa ‘Biology’, akajibu ‘ndiyo’. Hili ni swali linalohusu ufahamu na kwa wabibi wale ambao hawakwenda shule, hawajui biology ni nini. Si hivyo tu, hata wale walioishia darasa la saba hawajui biology ni kitu gani. Kuwauliza mabibi swali kama hili ni kuwadhalilisha kitaaluma kwa kuwa tu hawakwenda shule.
Bibi mwingine aliombwa amtongoze kijana yule anayewauliza maswali hadi amkubali. Bibi akatekeleza agizo hilo laivu mbele ya skrini ya TV! Huu ni udhalilishaji wa hali ya juu.
Kama kweli kinachofanyika katika kipindi kile ni kuwajali bibi wale kwa maana ya kuwapatia pesa wakishinda hebu wanaoendesha kipindi kile siku moja wawalete bibi zao na wawahoji maswali yale ya kishenzi tuone kama itakuwa sawa kwao, kwanini pesa iwe kigezo cha kudhalilisha watu wazima? Tena wanadhalilishwa na vijana wadogo wasio na chembe ya maadili? Hivi kweli kumwambia bibi mtu mzima amtongoze kijana mdogo halafu mbele ya skrini kila watu wa rika tofauti wanatazama wakiwemo watoto hapo tunafundisha maadili gani kwa jamii?
Wizara ya jinsia inapaswa kukataza udhalilishaji huu wa kijinsia. Nasi wananchi tuache kushabikia upumbavu huu–tukatae kuwapigia kura bibi wanaoshiriki
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?
Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...
-
Ee Mungu Mwenyezi uliyekubali Mwanao Yesu Kristu ateswe mpaka kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zangu naomba uwe nami. Ee Msal...
-
Josephine is passionate, dedicated, reliable, responsible, and hardworking. Team worker and able to face all challenging situations. Can ...
No comments:
Post a Comment