Never afraid to try on your own; No matter what, you can keep it real. Trust yourself...
03 May, 2014
YESU WAHI KURUDI! TAZAMA KIJANA HUYU ALIYEPANIA KUMUUA BABA YAKE MZAZI. SOMA MKASA MZIMA HAPA
DUNIA inaelekea kuzama.Katika tukio la kushangaza, kijana mmoja
aliyefahamika kwa jina la Anord Michael mkazi wa Mwenge jijini Dar es
Salaam, mwishoni mwa wiki iliyopita alifanya vurugu kubwa nyumbani kwao,
akidaiwa kutaka kumuua baba yake mzazi kwa sababu ambazo hazikueleweka
sawasawa.
Baba mzazi wa Anord Michael aliyedaiwa kutishiwa maisha na kijana wake
Huku majirani na watu wengine wakishangazwa na kitendo hicho, Anord
alimfungia ndani baba yake mzazi na kuanza kumshambulia kwa silaha
mbalimbali kabla ya kuchukua panga kwa lengo la kutaka kummaliza kabisa.
Polisi wakimdhibiti kijana Anord Michael
Mzee Michael, kuona kijana wake amepania kummaliza, alipiga mayowe ya
kuomba msaada, kitu ambacho kilifanikiwa kwani mara moja wasamaria wema
walijitokeza na kumuokoa kwa kumhifadhi katika chumba kingine ndani ya
nyumba hiyo.
Pamoja na hivyo, kijana huyo ambaye bado watu wana mashaka na utimamu
wa akili yake, aliendelea kufanya fujo huku akivunja mlango wa chumba
alichohifadhiwa baba yake ili aweze kumtoa roho, huku akitishia
kumuua mtu yeyote ambaye angejaribu kumsogelea.
Anord Michael akiwa mikononi mwa wanausalama
Akiwa katika hatua za mwisho kuvunja mlango huo huku baba yake naye
akianza kusali sala ya mwisho kabla ya mauti kumfika, ghafla askari
wenye silaha waliwasili eneo hilo na kuanza kumdhibiti kijana huyo.
Hata hivyo, zoezi la kumdhibiti kijana huyo halikuwa rahisi, kwani bado
alisababisha timbwili kubwa kabla ya maafande hao kutumia ujuzi wa
kikazi bila kutumia risasi na kumweka chini ya ulinzi.
Katika hali ya kushangaza, baada ya askari polisi kumuuliza sababu
iliyomfanya afikie uamuzi wa kumuua baba yake mzazi, Anord alidai mzee
huyo ndiye chanzo cha yeye kuharibikiwa kimaisha.
Baadaye maafande hao walimzoa kijana huyo na baba yake kuelekea Kituo cha Polisi Mabatini Kijitonyama kwa mahojiano zaidi.
No comments:
Post a Comment