24 September, 2014

JOHARI AWEKA WAZI UHUSIANO WAKE NA RAY

Msanii mkongwe wa filamu nchini, Blandina
Chagula maarufu kama Johari, ambaye ni ‘business partner’ wa msanii mwenzake, Vicent Kigosi aka Ray, amefunguka na kuzungumzia mahusiano yake na Ray pamoja na mipango yake ya kuolewa. Akizungumza na na chanzo makini cha kuaminika leo, Johari amesema anashangazwa kuwaona watu wakivumisha kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Ray.
“Mimi na Ray cha kwanza ni mtu na swahiba wake, cha pili ni kama kaka yangu kwasababu tumekaa kwa muda mrefu sana. Tumefanya kazi kama partner wangu, tuna ukaribu ambao upo kikazi zaidi na kampuni yetu, lakini uhusiano mwingine ambao watu wanauzungumzia sidhani kama upo ni maneno ya watu,” amesema. “Hatujawahi kutokea uhusiano wa kimapenzi na Ray. Unajua kuna watu wanaongea vitu vya kubuni, mimi na Ray tunafanya kazi kampuni moja na wote ni wakurugenzi kwahiyo inamaana tungekuwa tuna ugomvi tungevunja kampuni. kama hicho hakipo na bado tunafanya kazi vizuri na tunaheshimiana na kila mmoja kampuni inampatia maisha mazuri. Kwa sasa sijaolewa lakini siwezi kuweka wazi sana mahusiano yangu kwa sababu muda haujafika ila muda utakapofika Nitawaweka wazi.

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...