23 October, 2014

CATHY, KUBADILI JINA KISA LINA MKOSI

MKONGWE wa filamu kitambo, Sabrina Rupia ‘Cathy’ amesema kuwa jina analotumia katika sanaa lina mkosi hivyo yuko kwenye mkakati wa kulibadilisha na kujipa jina lingine labda linaweza kumkaa vizuri.

Staa wa filamu bongo Sabrina Rupia ‘Cathy'.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Cathy alisema anaona jina hilo lina mkosi kwa sababu linazungumzwa vibaya na baadhi ya wasanii wenzake hata kama kuna kitu ambacho hakijui ni lazima lihusishwe jina lake kitu ambacho anakiona kama jina hilo lina nuksi.
“Unajua naona jina hili lina mkosi kwa sababu kitu kilifanyika labda mimi nimepita tu basi litatajwa jina langu kitu ambacho mimi sikipendi na kuona labda lina matatizo jamani, haliko sawa kuendelea kuwa nalo,” alisema Cathy huku akidai yuko katika mikakati ya kutafuta jina lingine zuri ambalo anaona linamfaa zaidi.

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...