20 October, 2014

VIDEO: MTI ULIOANGUKA NA KUCHOMWA MOTO MIAKA 3 ILIYOPITA WASIMAMA GHAFLA!

10447627_721894961214173_1875934379784445685_nPichani ni mti unaodaiwa kunyanyuka ghafla baada ya kuanguka miaka mitatu iliyopitakatika kijiji cha Mfuto kata ya Ufuluma, iliyopo wilaya ya Uyuwi mkoani Tabora.

Katika hali ya kushangaza huku kila mtu akifikiria yake baada ya juzi huko  mkoani  Tabora, kutokea tukio la aina yake ambapo inaelezwa kuwa mti  aina ya Msufi uliokuwa  umeanguka yapata miaka  mitatu  iliyopita umesimama  ghafla  tena  kwa  sauti  kubwa ya  mrindimo na kuwafanya wananchi kujitokeza kwa wingi kushuhudia tukio hilo.

Tukio hilo limetokea  Oktoba 17,mwaka huu,katika kijiji cha Mfuto kata ya Ufuluma katika wilaya ya Uyuwi mkoani Tabora.

 Inaelezwa kuwa mti huo wenye kipenyo cha futi 2 uliinuka na kuwa kama zamani baada ya kutokea upepo mkali katika kijiji hicho.
Wananchi walikusanyika kila  mmoja akitaka kuchukua angalau gome la mti huo  kwa ajili ya  dawa ama kumbukumbu.

Mti huo ulioanguka na kuchomwa moto miaka 3 iliyo pita sasa wainuka na kusimama  wananchi wakaamua kuukata na kuchukua vipande vya mti huo kwa imani za kishirikina {kizimba}.Na maajabu mengine yakatokea ulipomalizwa mti na kubaki shimo ndani ya shimo pakawa na vitu vya thamani kama pesa nyingi,pingu za mjerumani n.k. Vilivyotumiwa na watu wa zamani.Watu wakachukua na kufanya shimo hilo kubaki jeupe,na hapo ndipo shimo hilo lilipoamua kuanza kulia kama binadamu.
TIZAMA VIDEO HAPA CHINI.




No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...