21 October, 2014

WAUMINI WALETA VURUGU WAKIMTUHUMU ASKOFU KUWA NI FREEMASON

              Askofu Boniface Kwangu

Waumini wa kanisa la Anglikana wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza walisimamisha kwa muda shughuli za ibada kanisani hapo baada ya kutokea vurugu kubwa.

Vurugu hizo zilitokea baada ya baadhi ya waumini hao kumtuhumu Askofu wa kanisa hilo Boniface Kwangu kwamba ni mmoja wa wafuasi wa kundi la Freemasons na hufanya kazi za kundi hilo!!

Mmoja wa waumini wa kanisa hilo Shadrack Lazaro alitoa tamko la jinsi askofu wao anavyofanya kazi la kundi la freemasons, ndipo waumini walipomvamia na kumtoa nje kwa nguvu na kusababisha vurugu kubwa.

Muumini huyo alisema pamoja na sababu kadhaa za kumkataa Askofu huyo, pia hawaridhishwi na tabia yake ikiwemo ya kutaka kubomoa sakafu akidai kuna hirizi imefichwa na baadhi ya waumini wake kanisani hapo.

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...