Rais Jakaya Kikwete (kushoto) alipokuwa anamnadi Edward Lowassa jimboni kwake Monduli 2010
The prime minister, who resigned, Edward Lowassa, has planned anytime from now, President Jakaya Kikwete kumkatia appeal.
The prime minister, who resigned, Edward Lowassa, has planned anytime from now, President Jakaya Kikwete kumkatia appeal.
The
meeting between Lowassa and the media, targeting citizens to sue
Kikwete for what he called, "defying the wishes of the majority."
Lowassa was among 38 members of the party were ripening in mbizo presidency, but his name was omitted in the initial stages. Kikwete was named kumuengua Lowassa for his personal interests.
WAZIRI mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, amepanga wakati wowote kutoka sasa, kumkatia rufaa Rais Jakaya Kikwete.
Taarifa
zilizopatikana jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki zinasema,
Lowassa amepanga kukutana na waandishi wa habari, Jumatatu au Jumanne
wiki hii.
Mkutano kati ya Lowassa na vyombo vya habari, unalenga kumshitaki
Kikwete kwa wananchi kwa kile kinachoitwa, “kukaidi matakwa ya wengi.”
Lowassa alikuwa miongoni mwa wanachama 38 wa chama hicho waliojitosa
katika mbizo za urais, lakini jina lake liliondolewa katika hatua za
awali. Kikwete ndiye anayetajwa kumuengua Lowassa kwa maslahi yake
binafsi.
“Ni kweli kwamba Edo (Edward Lowassa), amepanga kueleza kilichotokea
Dodoma kwenye mikutano ya chama chake. Atafanya hivyo kupitia mkutano
kati yake na waandishi wa habari,” ameeleza mmoja wa watu waliokaribu na
kiongozi huyo.
Hakuweza kufahamika mara moja, ikiwa Lowassa atautumia mkutano huo kueleza mustakabali wake wa baadaye wa kisiasa.
Hata hivyo, mwishoni mwa wiki, madiwani 20 kutoka jimboni kwake Monduli,
walitangaza kukihama CCM na kujiunga na Chadema; jambo ambalo linadaiwa
na wachambuzi wa kisiasa kuwa ni maandalizi ya mwanasiasa huyo
kukimbilia Chadema.
No comments:
Post a Comment