24 August, 2016

HII NDIO TAARIFA YA POLISI KUHUSU WANAOJIHUSISHA NA UKUTA


Licha ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kutangaza kufanya maandamano ya nchi nzima Septembe 1 2016, Jeshi la Polisi kanda maalum Dar es salaam limemkamata mtu mmoja anayejulikana kwa jina la Yoram Mbyellah kwa kupatikana na kuuza sare aina ya fulana zenye maneno yanayodaiwa kuwa ni yakichochezi zikiwa na alama ya CHADEMA huku nyingine zikiwa na maneno ‘UKUTA’
Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar es salaam Simon Sirro amesema…>>>’August 20 2016 Jeshi la Polisi lilipata taarifa toka kwa raia wema kuwa maeneo ya Kinondoni kuna duka linauza flana zenye maneno ya uchochezi yaliyoandikwa ‘’TUJIPANGE TUKATAE UDIKITETA UCHWARA’’ , ‘UKUTA’
Aidha Polisi baada ya kupata taarifa hizo walifika eneo la tukio na kumkamata mtuhumiwa aitwaye YORAM SETHY MBYELLAH miaka 42, mfanyabiashara na mkazi wa Mburahati akiwa anauza fulana hizo dukani kwake‘ –Kamanda Sirro
Ili tuishi kwa amani ni lazima tutii sheria na kama hutaki kutii sheria tutashughulika naye, Kama kuna mtu anataka kuvunja amani katika mkoa wetu ajue kabisa hatoweza na niseme tu kwamba kama wanataka kujenga ukuta wajenge ukuta mwingine maana huu umeshadondoka‘ –Kamanda Sirro
Na wapo watu wanasema kwanini tunafanya mazoezi, nikwamba Jeshi la Polisi ni kawaida kufanya hivyo na muhimu watu wajue hiyo September 1 hakutakuwa na maandamano ya aina yoyote kwahiyo watu wasiwe na hofu bali wachape kazi‘ –Kamanda Sirro

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...