Kinywaji cha coca cola kimeendelea kuwa maarufu duniani lakini
utafiti mpya umeonyesha kuwepo uhusiano wa kunywa sana kinywaji hicho na
matatizo ya uzazi kwa wanaume.
Kwa mjimu wa utafiti huo uliochapichwa kwenye Jarida la Epidemiology
la Marekani, wanaume wanaokunywa zaidi ya lita moja ya coca cola kwa
siku wanakabiliwa na hatari ya kuwa tasa.
Wanaume
waliotumia kinywaji hicho walikuwa na upungufu wa aslimia 30 ya mbegu za
uzazi zilizohesabiwa, ikilinganishwa na wale ambao hawakutumia. Wanaume
hao walionekana kuwa na matatizo ya uzazi zaidi kuliko wasiokunywa coca
cola.
No comments:
Post a Comment