22 October, 2014

VIDEO: HIVI NDIVYO KUKU WANAVYO ONGEZWA UNENE NDANI YA SEKUNDE 10 KWA KUTUMIA MABAKI YA NGURUWE!!







Waislam mpoooooooo........ Kwa wale wenzetu ambao nyama ya nguruwe ni dhambi kuila lakini kumbe huenda ukawa umeila bila kujua kupitia mabaki yake yanayotumika kuchakachulia kuku!!

Hii tamaa ya wafanyabiashara, ambayo haijali hata afya na maisha ya wateja wao inasikitisha sana. Baadhi ya kampuni zinazouza kuku, kama hii iliyonaswa kwenye video, zimestukiwa kuwa zinawajaza kuku wembamba ili kuwanenepesha na kuwaongeza uzito kabla ya kuwauza, kwa kutumia kimojawapo au mchanganyiko wa yafuatayo:
  1. Maji ya chumvi
  2. Kemikali za kuongeza ladha, na za kulainisha. Sababu kuku hao wamekuzwa haraka na kwa madawa, huwa hawana ladha ya asili
  3. Vimiminika/mabaki ya ng’ombe na nguruwe kutoka machinjoni
  4. Mwani au “seaweed” (mimea/magugu ya baharini)
seaweed mwani Kuku wanavyoongezwa unene kichakachuaji ndani ya sekunde 10, kwa kutumia mabaki ya nguruwe na vingine [Video]
Mwani (seaweed), mimea ya baharini ambayo ni mojawapo ya vinavyoongezwa katika uchakachuaji wa kuku
Ukiachilia mbali utapeli kwa wateja, uchakachuaji huu pia unahatarisha afya zao, na kudhulumu haki zao za kidini, kama mamilioni ya Waislam, na Wayahudi nchini Uingereza wanaokula kuku bila kujua kuwa kuku hao wameshindiliwa mabaki ya nguruwe (soma:Chicken injected with beef and pork waste sold in UK.) katika mchakachuo huu unaoitwa “chiken plumping”(nenepesha kuku,) kuku hao huongezwa takriban asilimia 30 ya uzito wao wa awali; karibia theluthi nzima. Video hapo juu zinaonyesha mojawapo ya mbinu na kifaa vinavyotumika katika uchakachuaji huo.

Mojawapo ya dalili inayoonyesha kuwa kuku amechakachuliwa, ni kusinyaa kwa kiasi kikubwa anapopikwa. Kwa muda baadhi ya wateja wa nchi mbalimbali za Ulaya na Asia walikuwa wanashangaa wanaponunua kuku mkubwa aliyenona, lakini mara baada ya kupikwa, wanasinyaa kuliko kawaida.
Kwenye video hapo juu, jamaa anaonyesha ni kiasi gani nyama ya kuku aliyonunua ilivyochakachuliwa. Aliweka nyama hiyo ya kifua cha kuku kwenye kikaango, bila mafuta wala maji, na kukipika kwa moto wa chini, na sasa analalamika na kuonyesha maji kibao yaliyotoka ndani ya nyama hiyo. Anasema ni Ulaya kusini, na Africa tu ambako amewahi kula kuku wazuri wa asili, na watamu. Lakini kuku wa Ulaya ya juu, USA, na Asia wanachakachuliwa zaidi

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...