- HII NI AIBU KWA WASOMI WETU WANAOSHINDWA KUTUMIA AKILI KWA KUENDEKEZA TAMAA ZISIZOKUWA NA FAIDA YOYOTE MBELE YA JAMII
Habari zilizopatikana kwa baadhi ya vijana ndani ya ukumbi wa mdahalo,
zinaeleza kuwa waliofanya vurugu waliahidiwa kulipwa fedha baada ya kazi
hiyo na kwamba, mkakati huo ulifanywa siku moja kabla ukiwahusisha
baadhi ya wanavyuo.
Baadhi ya wanafunzi waliohusika wanatoka vyuo vya Mwalimu Nyerere Kigamboni na Chuo cha Usimamizi wa Maji na Maendeleo.
Baadhi ya wanafunzi hao walitumiwa ujumbe wa kwenda kufanya vurugu na
mtu mwenye namba za simu 0656 501317 aliyejisajili kwa jina la Valence
Kisima.
Katika ujumbe wake, Kisima aliwaandikia aliokusudia wakafanye vurugu
kwamba; “Kesho Jumapili kuna kongamano Ubungo Plaza, mda (Muda) ni saa
sita, nauli ipo kwa mshiriki mpe taarifa na mwenzio.
Ujumbe mwingine wa Kisima ulieleza; “But asivae rangi ya chama kijani
wala njano coz 2kio ili ni maalum sana ntawapa maelekezo kesho saa tano
nikija ukumbini.
Waliyosema awali
Awali kabla ya vurugu kuanza, Warioba alisema Watanzania hawapaswi
kujivunia takwimu ya asilimia 81 ya masuala yaliyoingizwa katika katiba
iliyopendekezwa, kwa kile alichoeleza masuala muhimu yaliyokuwa na
nafasi ya kuleta mabadiliko yamewekwa pembeni.
Alisema mengi ya mambo yaliyoingizwa katika katiba hiyo ni yale mazuri
yaliyochukuliwa katika katiba ya sasa huku masuala ya msingi
yaliyopendekezwa na wananchi yakiwa yameachwa kando.
Aliongeza moja ya jukumu la tume aliyokuwa akiiongoza ni pamoja na
kuchukua mazuri ya katiba inayotumika sasa na maoni mengine ya wananchi,
huku akisema masuala ya tunu za taifa zilizoachwa na bunge maalum ni
muhimu kwa ajili ya mabadiliko.
Butiku, alisema watazunguka katika mikoa ya Mwanza Mbeya na nchi ya
Zanzibar, kwa ajili ya kufanya midahalo kama iliyofanyika katika maeneo
mengine chini.
Alisema mdahalo wa jana, unapaswa kutafsiriwa kuwa ni wa watanzania na si wa makundi kama ilivyokuwa awali.
Aliongeza kuwa wananchi wanapaswa kujua kilichomo ndani ya katiba hiyo,
japo bado haijasambazwa kwa kiasi kikubwa na kwamba, kwa sasa inapaswa
kujadiliwa na wananchi na siyo makundi.
“Tunataka mtaani katiba hii ijadiliwe pasipo kumuogopa mtu, hakuna
kusimamiwa na yeyote wala chama chochote, katiba hii ni yenu ili kesho
na kesho kutwa usije kumlaumu mtu au kulaumiwa na mjukuu wako kwa uamuzi
mtakaofikia baada ya kura ya maoni,” alisema Butiku.
Humphrey Pole pole, aliwaeleza wahudhuriaji kuwa katiba iliyopendekezwa
inapaswa kuangaliwa kwa umakini na kwamba, wananchi kuipigia kura ya
hapana siyo dhambi.
No comments:
Post a Comment