09 December, 2014

AFRIKA KUSINI: MWENDESHA MASHITAKA AMKABA KOO PISTORIUS


Oscar Pistorius .
Oscar Pistorius .
Mwendesha mashitaka anayejulikana kama  Gerrie Nel ameitaka  mahakama  iliyokuwa inasikiliza kesi ya Pistorius  kumuongezea adhabu kwa kile anachodai hukumu  aliyopewa  ni ndogo sana.
Jaji huyo Thokozile Masipa, aliahirisha kesi hiyo hadi siku ya Jumatano, akisema anataka muda zaidi kuchunguza tetesi zilizowasilishwa mahakamani na upande wa mashitaka ukitaka mahakama imuongfeze adhabu Pistorius.
Oscar Pistorius huenda akaachiliwa huru kutoka gerezani baada ya miezi kumi tu huku akitarajiwa kutumikia kifungo kilichosalia nyumbani.
Pistorius alifungwa jela miaka mitano mwezi oktoba kwa kosa la mauaji bila ya kukusudia na siku ya Jumatano mwendesha mashitaka atafahamu ikiwa anaweza kukata rufaa dhidi ya hukumu ya Pistorius.

No comments:

Post a Comment

UKIONDOA DIPLOMA, DEGREE AU PHD ULIYONAYO, KICHWA CHAKO KINABAKI NA NINI?

Horace Mann - Binadamu wa kwanza kugundua wazo la elimu Albert Einstein aliwahi kuulizwa akili ni nini? What is intellect? Akasema akili ni ...