Rais Robert Mugabe amemfuta kazi makamu wake Joice Mujuru, kufuatia ushindani wa uongozi katika chama tawala cha ZANU-PF.
Awali Bi Joyce Mujuru, anadaiwa kuwa yeye kuwa ni fisadi pamoja na kuhusika na njama ya kutaka kumuua rais Robert Mugabe.
Bi Mujuru alilaaniwa na Rais Mugabe wiki iliyopita na kuondolewa kutoka wadhifa wake wa makamu wa rais wa chama tawala cha ZANU-PF wakati wa kongamano la chama hicho mjini Harare.
Kwa upande wake Bi Munjuru amesema ameendelea kupokea vitisho na kuwa shirika la habari la serikali limeendelea kuchapisha habari za uongo za zisizo na msingi dhidi yake.
Katika hatua nyingine ilikuwa wiki nzima ya tuhuma dhidi ya Bi Mujuru kutoka kwa vyombo vya habari vya serikali kwa ushirikiano na mke wa Mugabe, Grace Mugabe, ambaye kwa sasa ameteuliwa kama afisaa mkuu wa chama cha ZANU-PF


No comments:
Post a Comment